Na John Walter-Manyara.
Mkuu wa mkoa wa Manyara Charles Makongoro Nyerere amekabidhi kikombe Cha na cheti Kampuni ya Mati Super Brands Ltd inayozalisha pombe Kali kwa kuwa mshindi katika Sherehe za Mei Mosi zilizofanyika uwanja wa Kwaraa mjini Babati.
Wameshinda katika vipengele vya Banda Bora na kwenye maandamano.
Zawadi hizo zimepokelewa na mkurugenzi wa Kampuni hiyo David Mulokozi.
Mbali na Mati Super Brand Ltd, wengine waliokabidhiwa zawadi ni Chuo Cha ufundi stadi Manyara (VETA) na Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira (BAWASA).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...