Ni desturi ya Meridianbet kurejesha kwa jamii na safari hii, siku maalumu ya kusherehekea
kinamama ilinogeshwa zaidi na kapu la bi mkubwa kutoka Meridianbet. Kama
wanavyotambulika kwa kuwa mabingwa wa Odds na Bonasi kubwa kwenye michezo ya
kubashiri, vivyo hivyo Meridianbet imewatambua na kuwaongezea tabasamu kinamama
wanaojishughulisha na kazi mbalimbali za kujipatia kipato.
Wapo wasusi, wavuvi, washonaji nguo, wauza mbogamboga, wauza
vyakula almaarufu ‘mama ntilie’ na wafanyabiashara wengine wengi wadogo wadogo.
Wote hawa ni sehemu ndogo ya kinamama wengi nchini wanaowekeza nguvu na muda
wao katika kazi ya kujipatia kipato ili kukidhi mahitaji yao na familia zao.
Kwa kutambua mchango na juhudi zao, Meridianbet ilifanya ziara fupi katika masoko ya Tandale, Manzese na Msasani jijini Dar es Salaam na kuwapongeza
baadhi ya kina mama wanaofanya shughuli zao ndogo ndogo kwenye maeneo hayo.
Akizungumza na Meridianbet baada ya kupokea zawadi kutoka kwenye
kampuni hiyo, mmoja ya kina mama hao (hakutaka jina lake kuwekwa hadharani),
ameishukuru Meridianbet kwa kuungana nao na kuwaongezea thamani kwenye majukumu yao.
Pamoja na hayo, ameiomba kampuni hiyo kuendelea kuifikia zaidi jamii na pia
kuwawezesha kinamama kwa kuwaongezea kwenye mitaji yao midogo ili waweze
kuzikuza biashara zao wanazozifanya.
Kwa upande wa Meridianbet, Afisa Mahusiano ya Jamii, Ndugu. Amani Maeda, amewapongeza kinamama wote nchini kwa kazi kubwa wanayoifanya hasa katika malezi ya jamii na, ameendelea kuwatia moyo kina mama wote wanaojishughulisha na kazi ndogondogo za kijikwamua kiuchumi. Bwana Maeda aliongezea kuwa, Meridianbet itaendelea kuwa karibu na jamii na itaendelea kuwafikia zaidi kwa kadiri itakavyowezekana.
Meridianbet, Nyumba Yenye Odds
Bora na Bonasi Kubwa!
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...