Na Said Mwishehe, Michuzi TV
RAIS
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania samia Suluhu Hassan ametoa rai kwa 
Watanzania wa sekta mbalimbali ikiwemo ya utalii kujitayarisha kupokea 
watalii watakaokuja kutalii nchini.
Ametoa rai hiyo leo Mei 
8,2022 wakati akizindua filamu ya Royol Tour katika Jiji la Dar es 
Salaam ikiwa ni siku chache tu baada ya kuzinduliwa rasmi nchini 
Marekani, kisha jijini  Arusha  na baadae Zanzibar.
“Mategemeo 
yangu  baada ya filamu hii kuzinduliwa Tanzania inatakiwa kujitayarisha 
kupokea wageni wengi, wageni watakuwa wa tofauti tofauti hizo hata 
watakapokuja watakaa katika hoteli za  tofauti.
“Hivyo nitoe  rai
 kwa sekta za utalii kujitayarisha ili watalii wakija wakute hoteli 
zipo, wakute watu wa kupokea wageni wapo, wapokea wageni viwanja vya 
ndege nao wajiandea.
“Zile sifa ambazo zimeoneshwa kwenye filamu 
lazima uonekane, tunapaswa kujitayarisha, watu wa sekta ya utalii na 
sekta nyingine tujitayarishe, narudia tena lazima Watanzania wote 
tujitayarishe,amesema Rais Samia.
Aidha amesema kuzinduliwa kwa 
Filamu ya Royol Tour ni mwanzo tu wa kuzindua filamu nyingine za Royal 
Tour awamu ya pili na ya tatu kwani kuna picha nyingi ambazo 
zilichukuliwa ambazo zitatumika kutengeza filamu nyingine kwa lengo la 
kendelea kutangaza utalii wa Tanzania.
“Filamu hii ya Royal Tour 
ni mwanzo tu kwani nyingine zitakuja.Nimpongeze Rais wa Zanzibar 
Dk.Hussein Mwinyi kwa ushiriki wake mzuri kwenye filamu hii na amekuwa 
na msemo wake kuwa yajayo yanafurahisha, hivyo tuseme yajayo 
yanafurahisha”amesema Rais Samia.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza wakati uzinduzi wa Filamu ya Tanzania'The Royal Tour' ambapo hafla ya Uzinduzi wa Filamu hiyo unafanyika Katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam leo Mei 8, 2022.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Hussein Ali Mwinyi, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa tayari wamewasili katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere tayari kwa ajili ya Uzinduzi wa Tanzania The Royal Tour ambapo mgeni rasmi ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.



















.jpeg)


.jpeg)

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...