

Baadhi ya watoa huduma za Mawasiliano katika Kanda ya Ziwa wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Dkt. Jabiri Bakari akiongoza kikao-kazi na watoa huduma katika kanda hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza tarehe 24 Mei, 2022, kujadili utendaji kazi na kusikiliza changamoto zinazoikabili sekta ya mawasiliano katika kanda ili kuzipatia ufumbuzi. Washiriki kutoka mikoa ya Mwanza, Kagera, Shinyanga, Geita, Mara na Simiyu wameshiriki kikao hicho. Picha na TCRA

Watoa huduma za mawasiliano katika Kanda ya Ziwa wakishiriki kikao kazi na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kilichoongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo Dkt. Jabiri Bakari na kufanyika katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza tarehe 24 Mei, 2022. Kikao hicho kililenga kujadili utendaji kazi wa watoa huduma katika kanda hiyo ambapo TCRA ilisikiliza na kupokea changamoto zinazoikabili sekta ya mawasiliano katika kanda ili kuzipatia ufumbuzi. Washiriki kutoka mikoa ya Mwanza, Kagera, Shinyanga, Geita, Mara na Simiyu wameshiriki kikao hicho. Watoa Huduma za Utangazaji kwa njia ya Redio, Televisheni na Mitandao, Televisheni za Kebo, Watoa Huduma za Mawasiliano ya Simu, Wamiliki wa Kampuni za Usafirishaji wa Vifurushi na Vipeto, Watoa Huduma za Intaneti pamoja na Umoja wa Mafundi Simu Kanda ya Ziwa. Picha na TCRA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...