Na Mwamvua Mwinyi, MAFIA
Mkuu
wa mkoa wa Pwani , Abubakari Kunenge ametoa Rai kwa wananchi
waliovamia na kuweka kambi za uvuvi katika kisiwa cha NYORORO ,wilaya
ya MAFIA kutii agizo la serikali kuhama mara moja katika kisiwa hicho .
Rai
hiyo imekuja kutokana na kisiwa hicho kuwa ni eneo tengefu kwa ajili ya
mazalia ya samaki katika bahari ya Hindi na sio vinginevyo.
Kunenge
alitoa rai hiyo wakati alipofanya ziara ya Kikazi katika kisiwa hicho
kukutana na wananchi hao ambao wamevamia kisiwa hicho ambacho hakina
huduma za kijamii na kuanzisha makambi ya kudumu.
Kwa
mujibu wa mkuu huyo wa mkoa, serikali kupitia kwa Waziri wa mifugo na
uvuvi Mashimba Ndaki tayari imeshakutana na wananchi na kuagiza
waondoke katika eneo hilo.
"Lakini
bado wameendelea kuwepo wanakaidi jambo ambalo limemlazimisha katibu
mkuu wa wizara hiyo kutoa maelekezo mengine kwa uongozi wa mkoa akiutaka
uongozi huo usimamie agizo la kuondolewa kwa watu hao";!
Amewataka
wananchi hao kuheshimu agizo hilo kwa kuwa nchi hii inaendeshwa kwa
misingi ya sheria na hakuna mtu yoyote aliyeko juu ya sheria,
Vilevile
aliwaasa, wananchi hao kupitia kwa mwenyekiti SAIDI LIKUWA kuunda
kamati ya watu watano wafike ofisini kwake ili kujadiliana namna
ambavyo wataweza kumaliza tatizo hilo kwakuwa serikali ya awamu ya sita
inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassani ni sikivu na ina wajali
wananchi wake.
Kwa upande
baadhi ya wakazi hao wameiomba serilali kuhalalisha kisiwa hicho kuwa
makazi ya watu na kuanzisha kitongopji ndani ya kisiwa hicho ili
wananchi waweze kupata huduma za kijamii .
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...