Na Amiri Kilagalila, Njombe
MAHAKAMA ya wilaya ya Makete mkoani Njombe imemuhukumu Faison Sanga (19) mkazi wa Makwaranga kata ya Ipelele kutumikia kifungo cha miaka 30 gerezani kwa kosa la ubakaji

Mnamo tarehe 12.2 2022 Bwana Faison sanga anatajwa kufanya kitendo hicho cha ubakaji kwa mwanafunzi wa shule ya msingi ( 15 ) .

Kosa hilo la ubakaji ni kinyume na kifungu cha 130 ( 1 ) ( 2 ) e na 131 ( 1 ) ya kanuni ya adhabu sura ya 16 Marejeo 2019 .

Aidha Bwana Sanga ameiomba mahakama kuweza kumpunguzia adhabu kwa kuwa ana familia inayomtegemea.

Kwa upande wa mashtaka uliiomba Mahakama kuweza kutoa adhabu kali ili iwe fundisho kwa wengine ambao wamekuwa wakikatisha masomo ya watoto wa kike.

Kwa upande wa mashtaka mashahidi wa kesi hiyo walikuwa wanne ambao ni muhanga mwenyewe,baba wa mtoto,Daktari kutoka hospitali ya wilaya ya Makete pamoja na G3615 Dictective Coplo Benedicto .

Hukumu hiyo imetolewa hapo jana na hakimu mkazi mfawidhi wilaya ya Makete Mh.Ivan Msaki pamoja na Inspecta wa jeshi la polisi Benstard Mwoshe Wilaya ya Makete.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...