Na Amiri Kilagalila
Mwenyekiti wa Chama Cha madereva wa IT (ITDA) wanaoendesha magari kutoka bandarini na kuyasafirisha kwenda nchi mbalimbali bwana Adam Mwenda ameishukuru mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) kwa kuendelea kutambua thamani ya madereva wanaotoa huduma hiyo ndani bandari baada ya mamlaka hiyo kuwapatia eneo litakalotumika kuwa sehemu rasmi ya kupumzikia madereva hao.

Akizungumza na waandishi wa habari akiwa kwenye ofisi za chama hicho zilizopo jengo la Maktaba ghorofa ya tatu jijini Dar es Salaam amesema, Aprili 29, mwaka huu wakati wa kikao kilichokuwakutanisha madereva wa ITDA na kamanda wa kikosi cha usalama barabarani nchini, SACP Wilbroad Mutafungwa kilichofanyika bandarini walitoa ombi kwa TPA juu ya eneo la kupumzika na kujihifadhi katika eneo namba mbili ndani ya bandari hiyo.
Aidha kufuatia ombi hilo hatimaye TPA imekubali kutoa eneo hilo na sasa ujenzi unaendelea wa kujenga viti na meza kwa kutumia saruji pamoja na kujenga bafu na choo vitakavyotumiwa na madereva hao.

“Hivi sasa ujenzi unaendelea, mafundi wameshajenga viti na meza vya zege pamoja na choo, kwa hiyo tunakwenda kutengeneza mradi mkubwa na heshima kubwa kwa madereva wote, kwa hiyo ni wakati mzuri kusema kwamba ITDA tunaweza kufanya mambo kwa ushirikiano na kushirikiana na taasisi zote za serikali na kuendelea kuaminika zaidi,” alisema Mwenda.
Mwenyekiti huyo ameishukuru TPA kwa kutoa eneo hilo na kueleza kuwa uamuzi huo hivi sasa unaleta imani kubwa kwao na kwamba sasa madereva wa ITDA wameanza kuonekana ni wathamani kubwa katika kusukuma gurudumu la maendeleo hapa nchini na ndiyo maana mamlaka hiyo imeamua kutoa eneo hilo.

“Nawaomba madereva kuwa wastaarabu wanapokwenda kwenye maeneo yale tukapumzike tukiwa na amani kabisa na tukiamini lile ni eneo letu sahihi  kwa mapumziko yetu  na pia kukaa pale bila kubughudhiwa,niwaombe wale wateja wanaokwenda kushoto na kulia tuwaeleze



 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...