Na Yeremias Ngerangera...Namtumbo


Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma imewagawia pikipiki 38 aina ya boxer zilizotolewa na wizara ya kilimo katika Halmashauri hiyo hivi karibuni.

Kaimu afisa kilimo katika Halmashauri hiyo Michael Gambi alisema kuwa pikipiki hizo 38 zimegawiwa kwa maafisa ugani pamoja na maafisa ushirika wa wilaya hiyo.

Gambi alidai taratibu za kugawa pikipiki hizo kwa maafisa ugani na ushirika wa wilaya hiyo umefanywa na mkuu wa wilaya ya Namtumbo Dkt Julius Kenneth Ningu ndiye

Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo Chiriku Hamisi Chilumba pamoja na kuipongeza serikali kwa pikipiki hizo alisema pikipiki hizo zitarahisisha utendaji kazi wa maafisa ugani na ushirika katika maeneo yao ya kazi kwa kutoa huduma ya ugani kwa ufasaha.

Chilumba alidai zipo changamoto za maafisa ugani za kutowafikia wananchi kwa wakati kutokana na tatizo la usafiri, hivyo kitendo cha serikali kutoa pikipiki hizo zitaondoa changamoto hiyo ya muda mrefu kwa maafisa ugani .

Mkuu wa wilaya ya Namtumbo Dkt Julius Kenneth Ningu pamoja na kuipongeza serikali kwa kununua pikipiki hizo aliwataka maafisa kilimo na ushirika kwenda kuchapa kazi kwa kutoa huduma bora kwa wakulima ili kuonesha tofauti katika uzalishaji wa mazao ya kilimo.

Ningu aliwataka maafisa kilimo na ushirika kuhakikisha pikipiki hizo zinafanya kazi iliyokusudiwa na serikali katika maeneo yao ya kazi na sio vinginevyo.

Wananchi wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo hujishughulisha sana na kilimo hivyo kutolewa kwa pikipiki hizo itarahisisha wataalamu wa kil.imo na ushirika kutoa huduma ya utaalamu wa kilimo kwa wananchi wa wilaya ya Namtumbo na kuongeza uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara katika wilaya hiyo.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...