Na Mwandishi Wetu,Lindi
MKUU wa Mkoa wa Lindi Zainab Telack ameiagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa( TAKUKURU) mkoani humo kufanya uchunguzi na kuwachukulia hatua ikiwemo kuwafikisha mahakamani waliohusika na ucheweshwaji wa ukamilishaji wa kazi katika mradi wa Barabara.
Barabara ambaazo zimecheleweshwa ni Uhuru,Msonabarini na mzunguko wa barabara ya Mchinga zilizojengwa Manispaa kwa kiwango cha lami .
Akizungumza leo na Baraza Maalumu la Madiwani Manispaa ya Lindi la kujadili taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2021-2022 Taleck ameishauri kuimarishwa kwa udhibiti wa ndani katika kusimamia utekelezaji wa mikataba.
Telack amesema Mhandisi Mshauri hakikishe anasimamia usimamizi wa karibu kwa wakandarasi ili kuweza kumaliza kazi iliyobaki katika mradi huo bila kuchelewa na kutoa huduma kwa wananchi .
Ametumia nafasi hiyo kueleza wazi waliohusika na ucheleweshwaji wa mradi huo wa Barabara uchunguzi ufanyike na kisha hatua ichukue mkondo wake ikiwa pamoja na kufikishwa kwenye vyombo vya Sheria ikiwemo Mahakamani.
Aidha amekemea tabia za baadhi ya wananchi kuchoma moto mashamba yao karibu na barabara na kuleta adha kwa watumiaji wa barabara na kulitaka Jeshi la polisi kufanya doria na kuwakama wale wote watakaochoma moto na kuwachukulia hatua za kisheria.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...