Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako ameongoza ujumbe wa nchi katika Mkutano wa 110 wa Kazi wa Kimataifa leo Juni 7, 2022 Geneva, Uswisi.

 

Aidha, Waziri Ndalichako ameshiriki pia kikao cha kundi la Afrika ambapo ametoa salamu za nchi na kuwaalika nchi wanachama wa Afrika na Duniani kote kutembelea nchi ya Tanzania kwa lengo kujionea Vivutio vya kitalii na shughuli za ustawi wa wananchi zinazotekelezwa vizuri na Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan. 

 



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako (wa pili kutoka kulia) akishiriki Mkutano wa 110 wa Kazi wa Kimataifa Juni 7, 2022 Geneva, Uswisi. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji Chama cha Waajiri Nchini, Bi. Suzanne Ndomba Doran, Naibu Mkuu wa Kituo Jiji la Geneva, Balozi Hoyce Temu. Kulia ni rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Bw. Tumaini Nyamhokia.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...