RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ameuagiza kila mkoa kutenga eneo litakalotumika kwa kilimo cha mazao yanayozalishwa katika mkoa husika.

Rais Samia ametoa agizo hilo leo wakati akihutubia kwenye kilele cha maadhimisho ya sikukuu ya wakulima (Nanenane) iliyofanyika katika uwanja wa John Mwakangale.

Aidha, Rais Samia amewataka wakulima kutumia maeneo hayo yatakayotengwa kuzalisha kibiashara ili kupata chakula cha kutosha na kuuza kwa nchi jirani.

Vile vile, Rais Samia amewataka wakulima kujisajili ili kupata vitambulisho ambavyo vitatumika kupata ruzuku ya mbolea kuendana na misimu.

Rais Samia pia amemuelekeza Waziri wa Mifugo na Uvuvi kushirikiana na Chuo cha Kilimo (SUA) ili kuwezesha vijana wanaohitimu chuoni hapo kuweza kujiajiri katika sekta hiyo.

Kwa upande mwingine, Rais Samia ameitaka Bodi ya Wakurugenzi na Uongozi wa NARCO kufanya uchambuzi wa vitalu vya ranchi vilivyokodishwa na kujua mapato yatokanayo na vitalu hivyo.

Halikadhalika, Rais Samia ameiagiza Wizari ya Mifugo na Uvuvi kufuta leseni za vitalu vilivyokodishwa na kupanga upya ili kufanya uwekezaji wenye tija.

Zuhura Yunus
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...