e906d57f3f0e0b6572c3fd432e303e17.png
 
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka Watanzania waendelee kuwa wazalendo kwa Taifa lao na washirikiane na Serikali katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
 
Ametoa kauli hiyo jana (Ijumaa, Agosti 05, 2022) wakati akizungumza na wakazi wa Ikungi alipokuwa katika ziara ya kikazi kataka wilaya ya Ikungi mkoani Singida.
 
“Nataka niwasihi msikwamishe maendeleo, lazima kila mmoja awe na uzalendo na wilaya yake, nawapongeza madiwani kwa mpango wenu wa kupanga mji huu.”
 
Waziri Mkuu alisema halmashauri ya wilaya hiyo imeweka mpango wa kuendeleza mji wake, wananchi ambao maeneo yao yatachukuliwa kupisha mradi huo watafidiwa kulingana na taratibu za uthamini.
 
Alisema Mthamini wa Serikali ana vigezo vya fidia, hivyo aliwasihi wananchi hao kuacha tabia ya kukataa kila mthamini anayekwenda kufanya uthamini katika eneo lao.
 
“Lazima mthamini mipango ya halmashauri yenu ya kuuboresha mji huu, isitokee mtu mmoja au wawili wakakwamisha maendeleo ya wenzao wa wilaya nzima.”
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...