Na John Walter-Babati.


Mahakama ya mkoa Manyara imemhukumu John Emmanuel (18) mkazi wa kijiji cha Malangi wilayani Babati kuchapwa viboko sita (6) baada ya kukutwa na kosa la ubakaji.


Hukumu hiyo ya kesi namba 73 ya mwaka 2021 imetolewa leo Septemba 26,2022 na Hakimu mkazi mkoa wa Manyara Mariam Rusewa.Hakimu Rusewa ameiambia mahakama hiyo kuwa Emmanuel alimbaka mwanafunzi wa darasa la nne (13) Septemba 10,2021 katika kijiji cha Malangi.


Kwa mujibu Kifungu cha 131 (2) cha sheria namba 16 kinaeleza kuwa, Bila kuathiri masharti ya sheria nyingine yoyote, ubakaji unapofanywa na mvulana wa miaka kumi na nane au chini; Kama mvulana huyo amefanya ubakaji kwa mara ya kwanza, atapewa adhabu ya viboko tu ambapo hakimu ataamua ni viboko vingapi.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...