Benki ya NMB inaendelea kutoa elimu kwa wafanyabiashara kwa lengo la kuhakikisha wanazielewa bidhaa na mipango ya benki hiyo ili wanufaike na biashara zao.

Akizungumza katika warsha ya klabu ya wafanyabiashara wa Mkoa wa Tabora, Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Magharibi, Sospeter Magese,alisema kikao na wafanyabiashara ni muhimu katika kubadilishana mawazo.

Magese alisema warsha hio ambayo haijafanyika tangu mwaka 2019 kutokana na ugonjwa wa UVIKO19, imekuwa na mafanikio makubwa kwa pande zote mbili na kuongeza kuwa wamepata fursa ya kuwaeleza wafanyabiashara bidhaa zao ikiwemo riba ya asilimia tisa katika kilimo.

Alieleza kuwa Benki ya NMB imechukua changamoto zote zilizotolewa na wafanyabiashara hao na kuahidi kuwa benki hiyo itazifanyia kazi haraka.

Naye Mwenyekiti wa Klabu ya wafanyabiashara hao,Michael Mambo,aliwataka wafanyabiashara kuacha uoga wa kukopa kutoka taasisi za fedha huku akisisitiza kuwa mikopo ina manufaa makubwa na iheshimiwe huku akiwasihi kutoitumia kinyume na malengo waliyokusudia.

Mfanyabiashara Elizabeth Nkonyoka alisema wamefurahi na kunufaika na warsha hiyo kwa kupata elimu ya kifedha na kujua masuluhisho mbalimbali ya kifedha ikiwemo umuhimu wa kulipa kodi.

Aliongeza kuwa wamenufaika na bidhaa za benki NMB na kushauri kuwa warsha kama hizo ziwe zinafanyika kila mwaka angalau mara moja.

Meneja wa benki ya NMB Kanda ya Magharibi, Sospeter Magese akizungumza na wafanyabishara wa Mkoa wa Tabora.
Mwenyekiti wa Klabu ya wafanyabishara Mkoa wa Tabora, Michael Mambo akifungua warsha hiyo iliyofanyika Mkoani Tabora.
Wafanyabishara katika warsha ya klabu ya wafanyabishara Mkoani Tabora iliyoandaliwa na benki ya NMB

 

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...