Katibu
 Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Hassan Abbasi, 
ametoa siku 7 kwa watendaji wa Idara ya Michezo kukamilisha nyaraka za 
miradi yote iliyoko chini ya Idara hiyo la sivyo kila mhusika atabeba 
mzigo wake.
Dkt. Abbasi ametoa agizo hilo leo hii alipokutana na 
watendaji wote wanaosimamia sekta ya michezo nchini kuanzia Idara ya 
Maendeleo ya Michezo iliyoko Wizarani, Chuo cha Maendeleo ya Michezo 
Malya na Baraza la Michezo (BMT). 
“Kuna changamoto kubwa sana za
 kiutendaji zilizobainika katika Idara ya Maendeleo ya Michezo kiasi cha
 kukwamisha miradi mingi nimekuja kuwaambia hapa nyie ndio wataalamu 
sisi tunatafuta hela kuna mabilioni ya fedha Serikali imetenga kila 
nyaraka unayouliza kazi zianze unaambiwa bado, kila kitu unachohitaji 
ukapewe hela Hazina hakijaandaliwa, sasa tumefanya mabadikiko ya uongozi
 wa juu wa Idara hii tunataka sasa kazi na matokeo na sio blah blah 
nyingi,” alisema Dkt. Abbasi.
Mtendaji Mkuu huyo wa Wizara ametoa
 siku saba kwa watendaji wanaokaimu katika Idara hiyo kukamilisha 
nyaraka hizo ikiwemo miradi ya ujenzi wa viwanja vya kupumzika wananchi,
 shule 56 za michezo na ukarabati wa viwanja mbalimbali vya michezo.
“Serikali
 inataka kazi na matokeo miradi yote hii mingi ishatengewa fedha na 
mingine tunahitajika kupata maandiko yenu wataalamu lakini kwa kiasi 
kikubwa imekuwa stori nyingi tu. Sasa baada ya siku 7 hizo kila 
atakayekwamisha tutampa jukumu analoonekana analiweza zaidi na si katika
 Idara hii muhimu kwa nchi ya maendeleo ya michezo,” alisema.
Wakati
 huo huo, Dkt. Abbasi jioni hii amefanya ziara ya kustukiza kwenye 
Baraza la Michezo nchini kukagua utekelezaji wa maelekezo ya kulitaka 
Baraza hilo kununua vitendea kazi mbalimbali vya kisasa yakiwemo magari 
kwa ajili ya kuboresha maslahi ya wafanyakazi.






Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...