Na Mwandishi wetu - Bungeni
Serikali ya Tanzania imesema haki ya faragha kwa wafungwa na wenza wao itaanza kutolewa pale ambapo sheria na miundombinu ya magereza itakapokidhi kutolewa kwa haki hiyo
Kauli hiyo imetolewa bungeni na Waziri wa Mambo ya Ndani Hamad Masauni alipokuwa akijibu maswali ya baadhi ya wabunge waliohoji ni lini wafungwa watapata haki hiyo
Waziri Masauni amesema masuala mengine yatakayozingatiwa kabla ya kuruhusiwa ni usalama, mila na desturi za Tanzania kwani haki hiyo inatakiwa kutekelezwa kwa faragha
Aidha amesema serikali inaendelea kutoa haki nyingine za msingi kwa wafungwa ikiwemo malazi, mavazi na chakula
"Tendo la ndoa ni haki lakini sio haki ya msingi, haki ya msingi ambayo tunatoa kwa wafungwa ni chakula, mavazi, malazi. Kuna mambo mengi ambayo yanapaswa kufanyika kwanza kabla ya kuruhusu haki hiyo gerezani" amesisitiza Waziri Masauni
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...