Na Mwandishi Wetu,Michuzi

MKUU wa Wilaya ya Kinondoni mkoani Dar es Salaam Godwin Gondwe leo Oktoba 26,mwaka 2022 amezindua ‘App’ mpya ambayo itafahamika kwa jina la Wese itakayokuwa ikiwezesha madereva kununua mafuta na kulipa baadae bila riba wala kamisheni.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa App ya Wese, Gondwe ameeleza kwamba Wese ni jukwaa la kifedha na biashara ambalo litakuwa  linaunganisha sekta ya uchukuzi, petroli na fedha.

"Huduma hii inatarajiwa kufanyiwa majaribio  katika Mkoa wa Dar es Salaam mwezi ujao , ikilenga kuwawezesha madereva wote wa magari makubwa, madogo, daladala, pikipiki na bajaji na wafanyabiashara kupata huduma ya mafuta kwa unafuu zaidi,"amesema.

Amoengeza  na  kuzinduliwa kwa ‘App’ hiyo kunakwenda  kuibua fursa kwa vijana wanaojihusisha na shughuli za usafirishaji.Aidha  mfumo wa kieletroniki utaenda kubadili maisha ya vijana na kuwajenga katika nidhamu ya  kutunza fedha na kukua kibiashara.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Mfumo wa Wese Francis Ekeng raia wa Nigeria amesema mfumo huo unafanana na mfumo kama wa taxi mtandao, ambao muhusika atalazimika kupakua ‘app’ hiyo kwenye simu yake ya kiganjani na kujisajili.

“Mtu akishajisaji atakuwa na uwezo wa kujaza mafuta ya gharama yoyote anayotaka katika kituo chochote cha mafuta nchi nzima, ila atatakiwa kulipa kabla ya saa sita usiku,” amesema.

Akifafanua zaidi anasema iwapo dereva atashindwa kulipa deni kwa wakati, atapigwa faini na iwapo atalipa kwa wakati atapata fursa ya kukidhi vigezo vya kukopesheka zaidi kutokana na uaminifu.

“Kila dereva anapochukua mafuta na kulipa bila kupata adhabu au kushindwa, pointi inatolewa ambayo inamjengea sifa yake ya kukopesheka zaidi,” amesema.Mkuu wa  Wilaya ya Kinondoni,Godwin Gondwe (kulia) akisalimiana  na Mwakilishi wa Mfumo wa Wese Francis Ekeng raia wa Nigeria leo Oktoba 26,mwaka 2022  Dar es Salaam.

Mkuu wa  Wilaya ya Kinondoni,Godwin Gondwe  akisoma hotuba yake wakati wa uzinduzi wa ‘App’ mpya ambayo itafahamika kwa jina la Wese leo Oktoba 26,mwaka 2022  Dar es Salaam.

Sehemu ya wadau wa Mafuta.





Mkuu wa  Wilaya ya Kinondoni,Godwin Gondwe akita katika picha za patoja na wanadau wa Mafuta.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...