Na Abel Paul wa Jeshi la Polisi

Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha Mrakibu wa Polisi SP SOLOMON MWANGAMILO amewataka madereva na wamiliki wa matrekta katika Mkoa wa Arusha kufuata sheria za usalama Barabarani Ili kupunguza ajali ama kumazimaliza ajali katika Mkoa huo.

SP Solomon Mwangamilo amesema hayo leo October 20 alipokuwa akizungumza na Madereva na wamiliki wa Matrekta katika kata ya Kikatiti wilaya ya Arumeru Mkoa Arusha ambapo amebainisha kuwa takwimu zinaonyesha kuwa ajali nyingi zinasabibishwa na vyombo hivyo kwa kukosa viakisi mwanga(reflectors).

Ametoa muda wa mwezi mmoja kufanya ukarabati wa vyombo hivyo nakuweka viakisi mwanga (reflectors) ili kupunguza ajali ambazo zina gharimu Maisha ya watu

Nao baadhi ya madereva na wamiliki wa vyombo hivyo wamesema semina na maelekezo waliyoyapata wameshapokea ambapo wamebainisha kuwa hapo mwanzo walikuwa hawana uelewa juu ya madhara ya kutoweka viaksi mwanga.






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...