Na Khadija   Kalili                
MKURUGENZI Mtendaji  Mradi wa 'Mbakiamturi Rice Project' Hamisi Kambanga amesema kuwa hivi sasa wanakabiliana na  shida ya ukosefu wa miundombinu  ya umwagiliaji hivyo wameiomba serikali kuwawezesha ili  waepukane  na kilimo cha kutegemea  mvua kwa sababu  wakilima kilimo cha umwagiliaji watakuwa na uhakika  w kuvuna  na kuzalisha mpunga mara mbili  kwa mwaka.

Mkurugenzi huyo amesema kuwa endapo wataendelea kulima kilimo cha kutegemea mvua  hawataweza  kujikwamua  na umasikin kwa sababu kilimo  kinakuwa  hakina uhakika  wa kuvuna  endapo mvua isiponyesha .       Amesema kuwa  mitaji inaweza kupotea  kwa sababu  mazao lazima  yatanyauka  kwahiyo ili kuweza  kupata suluhu ya changamoto hii  ni kuwawezesha kupata miundombinu  ya umwagiliaji  inayokadiriwa kugharimu  kiasi cha fedha Bil.3  kiasi ambacho kitahitajika katika awamu ya kwanza ya umwagiliaji kwa kumwagilia hekari 8,800. 

Mbakiamturi Rice  Project  ni wawekezaji vijana katika kilimo cha kisasa cha Mpunga  waliowekeza kwenye mashamba yaliyopo Wilayani  Kibiti Mkoani Pwani.   "Tunamuomba  Waziri wa Wizara  ya Kilimo  Mheshimiwa Hussein Bashe  afike katika mashamba yetu na kuweza kuona namna atakavyoweza kututatulia changamoto  mbalimbali tunazokabiliana nazo ikiwemo miundombinu mibovu ya namna ya ufikaji mashambani" amesema Kambanga.

Mkurugenzi huyo wa Mbakiamturi Rice Project amesema hayo  hivi karibuni  alipozungumza na kubainisha kuwa  licha ya  wamegubikwa  na changamoto nyingi  ikiwemo ukosefu wa  barabara,  maji mawasiliano ya mtandao.

"Ukiwa  kijijini  huwezi kufanya jambo  lako kwa sababu namna ya ufikaji  mjini kufuata mahitaji muhimu  nauli kwenda na kurudi inagharimu Sh. 50,000  kwa njia ya usafiri wa  pikipiki  jambo ambalo limekua  changamoto kubwa tunazokabiliana nazo , pia hakuna mitandao (Internet)   tunahitaji mitandao kwa sababu hivi sasa dunia ni kijiji pia huduma zote zinapatikana kwa njia ya mtandao.
Mkurugenzi  Mkuu wa Mbakiamturi  Rice Project, Hamisi.Kambanga mradi huo uliopo Wilayani Kibiti Mkoani Pwani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...