TIMU ya Taifa ya Wanawake chini ya miaka 17 (Serengeti Girls) jioni ya  Oktoba 14, 2022 wamefanya mazoezi ya mwisho kuelekea mchezo wao na Ufaransa utakaochezwa saa 4: 30 jioni  saa za nchini India, Oktoba 15  Uwanja wa Pandit Jawaharlal Nehru jijini Goa.

Baada ya Mazoezi Kocha wa timu Bakari Shime ameeleza kuwa hali ya wachezaji iko vizuri, morali ya kupambana ipo kwa ajili ya taifa.

Naye Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo la Taifa ( BMT) ameshuhudia mazoezi hayo na kusema wachezaji wana ari, na mazoezi wamefanya vizuri na wanaoenakana wako tayari kuikabili Ufaransa na baadae mechi dhidi ya Canada.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...