Na Mwandishi Wetu, 

WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Stergomena Tax ameshiriki  kwenye Jukwaa la Uchumi kati ya Ureno na Tanzania lililofanyika jijini Lisbon,   Ureno.

Kupitia jukwaa hilo, Mhe. Stergomena Tax amewakaribisha wawekezaji kutoka Ureno kuchangamkia fursa za uwekezaji kwenye sekta zenye kipaumbele nchini  Tanzania zikiwemo sekta za kilimo, utalii, miundombinu na uchumi wa buluu. 

Aidha Waziri Tax ameelezea  uwepo wa mazingira mazuri   yanayorahisisha shughuli za uwekezaji na kibiashara kwa makampuni yanayokuja kuwekeza nchini Tanzania. Jukwaa hilo liliandaliwa na Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Ureno wenye makazi yake Paris, Ufaransa,  kwa kushirikiana na Wizara ya  Mambo ya nje ya Ureno na Wizara  ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki  wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 

Jukwaa hilo  lilihudhuriwa pia na Naibu Waziri wa Biashara za Kimataifa na Uwekezaji wa Ureno na wawakilishi kutoka Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Mamlaka ya Kukuza Uwekezaji Zanzibar (ZIPA) na Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Ureno (AICEP).

Jukwaa hilo limeandaliwa kwa ajili ya kuanisha fursa za uwekezaji nchini Tanzania lakini pia kutafuta masoko ya bidhaa za Tanzania nchini Ureno.
Mhe. Dkt. Stergomena L. Tax (Mb.), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, akifuatilia moja ya wasilisho kuhusu fursa za uwekezaji nchini Tanzania. Kulia kwake ni Mhe. Bernado Ivo Cruz, Naibu Waziri wa Biashara ya Kimataifa na Uwekezaji wa Nje. Kushoto kwake ni Bw. Luis Castro Henriques, Mwenyekiti na Mkurugenzi Mtendaji wa Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Ureno, AICEP

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...