Kampuni inayojishughulisha na utengenezaji wa vifaa vya ujenzi ya Knauf Gypsum Tanzania imesema mazingira ya uwekezaji hapa nchini yameboreka kwa kiasi kikubwa na kutangaza kuwekeza shilingi bilioni 115 katika upanuzi wa kiwanda chake kilichopo Mkuranga mkoani Pwani.

Kampuni hiyo yenye asili ya Ujerumani tayari imeshawekeza kiasi cha shilingi bilioni 163 hapa nchini kwenye kiwanda na uzalishaji wa vifaa mbali mbali vya ujenzi wa nyumba ikiwamo gypsum na imesema itawekeza kiasi kingine cha shilingi bilioni 115 kufikia mwaka 2025.

Akiongea wakati wa halfa ya chakula cha jioni kilichoandaliwa kwa ajili ya kuwashukuru wateja wake na wadau mbali mbali, Mkurugenzi wa Knauf ukanda wa Afrika Mashariki Ilse Boshoff aliishukuru serikali, wateja na wadau mbali mbali kwa kuifanya safari ya uwekezaji wa kampuni hiyo hapa Tanzania yenye mafanikio.

Kila kunapokucha kampuni ya Knauf inapiga hatua kadhaa mbele. Historia yetu kwa hapa Tanzania ilianza mwaka 2014 tulipofungua ofisi na baadaye kuanzisha Kampuni ya Knauf Gypsum Tanzania na kuanza kazi rasmi mwaka 2017,” alisema.

Mkurugenzi huyo alifafanua kuwa mwaka 2018 kampuni hiyo ilianza ujenzi wa kiwanda cha kisasa kilichopo Mkuranga mkoani Pwani na mwaka 2020 kilianza uzalishaji kikiwa na uwezo wa kuzalisha mita za mraba milioni 15 kwa mwaka.

Akitangaza uwekezaji zaidi katika kiwanda hicho alisema.,“Uwezo wa uzalishaji kwa kiwanda cha Mkuranga ni mita za mraba milioni 15 kwa mwaka na malengo yetu ni kukipanua na kukiwezesha kuzalisha mita za mraba milioni 43 kwa mwaka kufikia mwaka 2025. Uwekezaji huu utagharimu shilingi bilioni 115,”

Aliongeza kuwa upanuzi huo utakifanya kiwanda hicho kuwa kikubwa kuliko vyote kwa Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika na pia utakifanya kiweze kuongeza usafirishahi wa vifaa inavyozalisha nje ya Tanzania kwa asilimia 170.

Dickson Mtekere, mmoja kati ya wateja wa Knauf aliyehudhuria hafla hiyo kutoka kampuni ya Shananga Group Limited ya Dar es Salaam aliishukuru Knauf kwa kuweza kuwakutanisdha wateja wake na kutambua mchango wao katika kuongeza soko la bidhaa zinazotengenezwa kwa malighafi za Kitanzania zikitumia teknalojia ya kisasa kutoka nchini Ujerumani.

“Naishukuru Knauf kwa kutukutanisha wateja wake na kutambua mchango wetu. Uwekezaji wa kampuni hii umetusaidia sana sisi wafanyabiashara kwa kuwa wanatengeneza bidhaa ambazo kabla ya kuja kwake tulilazimika kuziagiza nje ya nchi kwa gharama kubwa huku tukipoteza muda mwingi. Ni wazi kuwa upanuzi wa kiwanda cha Mkuranga utaongeza fursa za kibiashara na ajira kwa Watanzania,” alisema

Mkurugenzi  Mtendaji wa Kampuni ya Knauf Gypsum Tanzania inajishughulisha na utengenezaji na uuzaji wa vifaa vya ujenzi  Ilse Boshoff (kulia) na meneja masoko wa kampuni hiyo Lilian Mangaru (kushoto) wakimkabidhi mkurugenzi wa kampuni ya  Super Terrazzo Ltd Nish Hiran tuzo baada ya kuibuka mshindi  wa usambazaji wa bidhaa za kampuni hiyo katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

Mkurugenzi  Mtendaji wa Kampuni ya Knauf Gypsum Tanzania inajishughulisha na utengenezaji na uuzaji wa vifaa vya ujenzi  Ilse Boshoff (kulia) akimkabidhi cheti mwakilishi wa duka la kuuza vifaa vya ujenzi la Shanoga Hardware  la Dar es Salaam Anna Kijugu cheti ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wa duka hilo katika kuuza bidhaa za ujenzi zilizotengenezwa na malighafi za ndani zinazotengenezwa na kapuni hiyo. Anayeshuhudia kushoto ni Meneja Masoko (Marketing manager) wa Knauf Lilian Mangaru.

Mkurugenzi  Mtendaji wa Kampuni ya Knauf Gypsum Tanzania inajishughulisha na utengenezaji na uuzaji wa vifaa vya ujenzi  Ilse Boshoff (kulia) akishuhudia Meneja masoko wa kampuni hiyo Lilian Mangaru (kushoto) akimkabidhi tuzo mmoja wa wateja wa kampuni hiyo Dickson Mtekere kutoka kampuni ya Shananga Group Limited ya Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya kutambua wa kampuni hiyo katika kuuza bidhaa za ujenzi zilizotengenezwa na malighafi za ndani na kampuni ya Knauf.


Baadhi ya wateja wa wa Kampuni ya Knauf Gypsum Tanzania inajishughulisha na utengenezaji na uuzaji wa vifaa vya ujenzi  wakiwa katika picha ya pamoja na uongozi wa kampuni hiyo muda mfupi baada ya kukabidhiwa tuzo za kutambua mchango wao katika 



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...