Mkuu wa Mkoa wa Mara, Meja Generali Suleiman Mzee (kulia), akioneshwa na Kamishna Msaidizi wa Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha, Bi. Dionisia Mjema (wapili kulia), mabanda mbalimbali yaliyopo katika Mtaa wa Benki katika maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa, yanayoendelea katika Viwanja vya Rock City Mall, jijini Mwanza, wapili kulia ni Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza, Bw. Balandya Elikana na kushoto ni Mchumi Mwandamizi kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Ikunda Rumisha.
Mkuu wa Mkoa wa Mara, Meja Generali Suleiman Mzee, akioneshwa mifumo ya malipo na Kamishna Msaidizi wa Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha, Bi. Dionisia Mjema, alipotembelea katika maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa, yanayoendelea katika Viwanja vya Rock City Mall, jijini Mwanza.
Mkuu wa Mkoa wa Mara, Meja Generali Suleiman Mzee, akizungumza na Kamishna Msaidizi wa Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha, Bi. Dionisia Mjema, alipotembelea katika maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa, yanayoendelea katika Viwanja vya Rock City Mall jijini Mwanza.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Wizara ya Fedha na Mipango, Mwanza)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...