Baadhi ya Picha za washiriki wa kongamano la pili la  Afya la Sayansi Shirikishi kuhusu Vimelea Sugu vya Magonjwa dhidi ya Dawa lililofanyika jijini  Dar es Salaam.
Baadhi washiriki wakipata maelezo kuhusiana na Mradi wa HPSS Tuimarishe Afya kwenye kongamano la pili la  Afya la Sayansi Shirikishi kuhusu Vimelea Sugu vya Magonjwa dhidi ya Dawa lililofanyika jijini  Dar es Salaam.



Na Chalila Kibuda MichuzI TV

SERIKALI imetoa tahadhari kuhusu matumizi mabaya ya dawa za antibiotiki ambapo imesema kuwa matumzi holela ya dawa hizo husababisha usugu wa vimelea dhidi ya dawa hali inayoweza kusababisha kupoteza Maisha ya watu na wanyama.

Kauli hiyo imetolewa na Mganga  Mkuu wa Serikali Profesa Tumaini Nagu kwa niaba ya Waziri wa Afya ,Ummy Mwalimu  wakati  akifungua Kongamano la pili la Afya ya Sayansi Shirikishi kuhusu usugu wa vimelea dhidi ya dawa iliyofanyika Dar es Salaam.

Prof Nagu amesema takwimu za tafiti zinaonesha kuwa matumizi ya dawa za antibiotiki nchini ni asilimia 92 sambamba na usugu wa asilimia 59.8 ambapo makadirio yanatazamiwa kuwa makubwa katika sekta ya uvivu na mifugo kutokana na utafiti kuonesha asilimia 90 hutumia dawa za antibitiki kutibu wanyama badala ya chanjo.

 “Leo tuna matukio matatu kwanza ni kutambulisha mpango kazi wa taifa wa kupambana na usugu wa vimelea dhidi ya dawa, pili ni maadhimisho ya wiki ya usugu wa vimelea dhidi ya dawa na tatu  ni kupokea taarifa ya utekelezaji wa mpango kazi wa taifa juu ya mapambano ya usugu wa vimelea dhidi ya dawa (2017/2022).

Amesema Tanzania kama zilivyo nchi nyingine Duniani kwa kiasi kikubwa inakabiliwa na janga la usugu wa vimelea  dhidi ya dawa katika mapambano serikali inatekeleza mkakati wa 68 wa kidunia  wa mkutano wa afya duniani wa 2025 .

Amesma Wizara za Afya, Mifugo na Uvuvi, na Kilimo kupitia Kamati ya Kitaifa ya Kuratibu shughuri za Kuzuia Usugu wa vimelea  Dhidi ya Dawa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali zimeweka mikakati mbalimbali ili kukabiliana na changamoto zinazotakana na usigu wa vimelea dhidi ya dawa.

Wadau wa maswala ya afya waliokuwepo katika kongamano hilo ni Mradi wa HPSS Tuimarishe Afya, vyuo vikuu na taasisi za utafiti ambao ndi wamefanikisha  kongamano.

Amesema Kongamano hili linafanyika katika Wiki ya Kimataifa ya Mapambano dhidi ya Usugu wa Dawa, ambayo hufanyika kote duniani kuanzia tarehe 18 Novemba hadi tarehe 24 Novemba kila mwaka.
 
Dk Karin Wiedenmayer, Mtaalamu Mwandamizi wa Afya ya Umma na Dawa katika Mradi wa HPSS amesema  kongamano  la  kwanza kuhusu usugu wa dawa nchini liliandaliwa na mradi wa HPSS Tuimarishe Afya mnamo mwaka 2017 na likawa na mafanikio makubwa.
 
“Baada ya miaka mitano tangu tuandae kongamano la kwanza tunafurahi kuona kwamba wazo letu sasa limechukuliwa kikamilifu na serikali.''
 
Dk.  Wiedenmayer piaa alipongeza Serikali na wadau  kwa jitihada zao kubwa za kushughulikia na kupunguza madhara ya usugu wa dawa nchiniTanzania.

HPSS Tuimarishe Afya ni mradi wa Ushirikiano kati ya Serikali za Uswizi na Tanzania, unaofadhiliwa na Serikali ya Uswizi na kutekelezwa na Taasisi ya Uswisi ya Tropical and Public Health Institute

Dk.Karin amesema Usugu wa dawa ni mojawapo wa matishio makubwa ya afya ya umma duniani ambayo huperekea kuwa vigumu kutibu maambukizi ya magonjwa ya kawaida na hivyo kuongeza hatari ya kuenea kwa magonjwa hayo na vifo.

Dk Karin Wiedenmayer, Mtaalamu Mwandamizi wa Afya ya Umma na Dawa katika Mradi wa HPSS.

Mtaalamu Mwandamizi wa Afya ya Umma na Dawa katika Mradi wa HPSS Dk Karin Wiedenmayer akitoa maelezo kuhusiana na Mradi wa HPSS inavyoshiriki katika mapambano ya vimelea sugu vya magonjwa dhidi ya dawa katika kongamano la pili la  Afya la Sayansi Shirikishi lililofanyika jijini  Dar es Salaam.
Mfamasia Mkuu wa Serikali Daud Msasi akitoa maelezo   kuhusiana na kongamano la pili la  Afya la Sayansi Shirikishi kuhusu Vimelea Sugu vya Magonjwa dhidi ya Dawa lililofanyika jijini  Dar es Salaam.
Mganga Mkuu wa Serikali Profesa Tumaini Nagu akizungumza wakati akifungua kongamano la pili la  Afya la Sayansi Shirikishi kuhusu Vimelea Sugu vya Magonjwa dhidi ya Dawa lililofanyika jijini  Dar es Salaam.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...