Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Viongozi pamoja na Wanachama wa Chama cha Menejimenti ya Kumbukumbu na Nyaraka Tanzania (TRAMPA) kabla ya kufungua Mkutano wa 10 wa Chama hicho uliofanyika kwenye ukumbi wa Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC) tarehe 27 Novemba, 2022.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea
Tuzo ya Heshima kutokana na mchango wake katika kada ya uwekaji wa
Kumbukumbu na Nyaraka mara baada ya kufungua Mkutano wa 10 wa Chama cha
Menejimenti na Kumbukumbuku na Nyaraka Tanzania uliofanyika kwenye
ukumbi wa Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC) tarehe 27
Novemba, 2022.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na viongozi wa Chama cha Menejimenti ya Kumbukumbu na Nyaraka Tanzania (TRAMPA) katika picha ya pamoja na Wanachama wa Chama hicho mara baada ya kufungua Mkutano wa 10 wa Chama hicho uliofanyika kwenye ukumbi wa Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC) tarehe 27 Novemba, 2022.
Wanachama wa Chama cha Menejimenti ya Kumbukumbu na Nyaraka Tanzania (TRAMPA) pamoja na Wageni wengine wakimsikiliza mgeni Rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan wakati akiwahutubia kabla ya kufungua Mkutano wa 10 wa Chama hicho uliofanyika kwenye ukumbi wa Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC) tarehe 27 Novemba, 2022.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...