Njombe

Mahakama ya Hakimu mkazi Njombe imeahirisha kesi No 2,2022 ya madai ya fidia ya shilingi Mil 100 iliyofunguliwa na msimamizi wa mirathi wa marehemu Kaselida Mlowe dhidi ya kanisa la kiinjili la kirutheli Tanzania Dayosisi ya kusini mpaka February 17 kutokana na hakimu mfawidhi wa Mahakakama hiyo kuwa safarini.

Mahakama imeahirisha kesi hiyo ya madai iliyofunguliwa na msimamizi wa mirathi baada ya mlalamikaji kushinda trafic kesi no 6 ,2021 iliyotokea eneo la Kibena katika mlima Ichunilo septemba 25,2020 iliyohusisha gari aina ya Hiace yenye nambari za usajiri T298-DNE na gari aina ya Mercedez Benz Truck yenye nambari za usajiri T210-AHU mali ya kanisa ambayo ilipelekea kifo cha Kaselida Karo Mlowe ambaye aliacha watoto wadogo watatu.

Katika kesi ya kwanza ya ajali ya barabarani iliyosimamiwa na hakimu wa wilaya ya Njombe Matrida Kayobo iliyosababisha majeruhi na kupelekea kifo cha Kaselida Mlowe,Mahakama ilimkuta na hatia dereva aliyekuwa akiendesha gari hiyo ya kanisa hatua iliyompa mamlaka mlalamikaji ya kufungua kesi ya fidia dhidi ya mlalamikiwa ili kusaidia watoto walioachwa na Marehemu.

Akizungumzia hatua hiyo wakili wa upande wa mlalamikaji Gervas Semgamo kwa niaba ya mawikili Emmanuel Chengula na Frank Ngafumika amesema baada ya hatua mbalimbali ya matakwa ya keshiria juu ya shauri hilo kesi hiyo ya madai ilitarajiwa kuanza kusikilizwa tarehe 3 lakini imeweza kuahirishwa mpaka tarehe 17.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...