Mkurugenzi wa ZEEA Mh. Juma Burhani,Mkurugenzi wa SMIDA Mh. Soud Said Ali na Mkurugenzi Mtendaji wa Equity bank (T) Bi. Isabela Maganga wakionesha umma nyaraka baada ya kusaini makubaliano ya kufanya kazi kwa pamoja leo katika ukumbi wa Golden Tulip Zanzibar. Hafla hiyo ilihudhuriwa na Waziri wa nchi Ofisi ya Raisi,kazi,uchumi na uwekezaji mh. Mudrick Soraga.[
 Waziri Wa Nchi Ofisi Ya Raisi, Kazi, Uchumi Na Uwekezaji Mh. Mudrick 
Soraga Akitoa Neno Kwenye Hafla Hiyo Akiwa Kama Mgeni Rasmi Benki ya Equity Tanzania imeingia makubaliano ya kufanya kazi na taasisi ya ZEEA pamoja na SMIDA za Zanzibar kwa lengo la kuhakikisha wanatoa mikopo nafuu kwa wajasiriamali wakubwa na wadogo na kuwapa elimu za kifedha kama sehemu ya mkakati wa benki kuhakikisha wanatoa huduma bora na gharama nafuu kwa kila Mtanzania.
Makubaliano
 ya kufanya kazi kwa ushirikiano baina ya ZEEA na SMIDA ambapo Equity 
kama benki wanakwenda kutoa mikopo bila riba kwa jamii ya wazanzibari, 
Makubaliano haya yanakwenda kuleta mageuzi makubwa sana katika sekta ya 
fedha na uchumi kwani yatawezesha taasisi zetu kuleta maendeleo ya 
haraka kwa vijana, si tu maendeleo bali kukuza elimu ya fedha na ukopaji
 wenye malengo na tija.Makubaliano haya yatasaidia katika suala zima la 
kuongeza ajira kupitia nguzo ya ujasiliamali kwani wajasiliamali 
watapata mitaji ya kutosha kukuza biashara zao sambamba na kuongeza 
ubunifu. Ili kufikiwa matamanio haya, Benki ya Equity itakuwa na mengi 
na mahususi ambayo ni pamoja na:-
Kutumia miundombinu ya kibenki katika kuwezesha utoaji wa mikopo ambayo imethibitika, hii ni pamoja na mifumo na rasilimali watu Kutumia uzoefu wa ufuatiliaji mikopo ili kuhakikisha kuwa pesa inayokopeshwa pasi na riba inarejeshwa kwa wakati na kulingana na vigezo na masharti yaliyokubaliwa Kutoa taarifa kwa vyombo wabia (ZEEA na SMIDA) juu ya ufanisi wa program hii kwa wakati.
Kutoa mikopo kwa wakati (ndani ya siku 14 za kazi) Kuendelea kutoa mikopo bila riba wakati wote program hii kwa wajasiriamali katika Nyanja zote za uzalishaji.
Kutumia mtaji wake katika kufanikisha program hii ya kukopesha wajasiriamali bila riba
Aidha
 benki itaendelea kutoa elimu ya fedha kwa vikundi na mtu mmoja mmoja 
kwa gharama zake na kuhakisha inaongeza uchumi shirikishi ili kuongeza 
kipato cha mzanzibari mmoja mmoja.Hafla iyo iliyohudhuliwa na waziri wa 
nchi ofisi ya raisi,kazi.uchumi na uwekezaji Mh Mudrick Soraga. 
Mkurugenzi mtendaji wa Equity Bi Isabela Maganga alimuhakikishia waziri 
kuunga mkono juhudi kubwa zinazofanywa na Mh. Rais wa Zanzibar 
(Dr.Husein All Mwinyi) na zile za Mh.Rais wa Jamhuri ya Muungano 
Tanzania (Dr.Samia Suluhu). 





Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...