NA MWANDISHI WETU, LUSHOTO
WAJUMBE
wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii, wametembelea
kiwanda cha kuchakata Chai Mponde kilichoko Wilaya ya Lushoto Mkoani Tanga
Machi 16, 2023 ili kukagua utekelezaji wa miradi mitano inayotekelezwa na Ofisi
ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu (OWM-KVAU) na taasisi
zilizo chini yake.
Kiwanda
cha Chai Mponde kinamilikiwa kwa ubia na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kwa
Watumishi wa Umma (PSSSF) na Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) taassi ambazo
ziko chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu
(OWK-KVAU), kila taasisi inamiliki
asilimia 42% ya hisa na Msajili wa Hazina(TR) asilimia 16%.
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu, Mhe.
Profesa Joyce Ndalichako, Naibu wake Mhe. Patrobas Katambi, Katibu Mkuu Profesa
Jamal Katundu na Wakurugenzi Wakuu wa Taasisi hizo, CPA. Hosea Kashimba (PSSSF)
na Dkt. John Mduma (WCF) pia walikuwepo wakati wa ziara hiyo.
Kiwanda
cha Chai Mponde kilifanyiwa ukarabati mkubwa baada ya kusimama kufanya kazi kwa
zaidi ya miaka 10 hali iliyosababisha mitambo na majengo kuchakaa sana.
Hali
hiyo iliifanya Serikali kutafuta njia ya kukifufua kiwanda hicho ili kiweze
kuwanufaisha wakulima wa Chai wa Halmashauri ya Bumbuli na wilaya ya Lushoto
kwa ujumla wake, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na
Wenye Ulemavu, Profesa Joyce Ndalichako alisema.
Baada
ya uwekezaji mkubwa uliofanyika kiwanda kimeanza kazi ambapo kilo 24,460
zimeuzwa na tani 50 zinategemewa kuuzwa mwishoni mwa mwezi Machi, 2023, Meneja
wa kiwanda hicho, Sane Kwilabya alisema.
Wajumbe
hao wa Kamati walitembezwa maeneo mbalimbali ya kiwanda kuanzia sehemu ya
kupokelea majani ya chai kutoka kwa wakulima, sehemu ya kunyausha (Withering),
jinsi majani ya chai yanavyochakatwa (Processing) na kupata aina mbalimbali za
unga wa chai iliyochakatwa (grading) sehemu ya Boiler inayotumika kukaushia
chai (Dryer), sehemu ya kuhifadhi magogo ya miti na sehemu inayotenganisha chai
iliyochakatwa kulingana na madaraja mbalimbali (ukubwa wa chengachenga za chai)
Aidha
baada ya wajumbe kutembelea kiwanda na kupatiwa maelezo ya kina kuhusu
uendeshaji wa kiwanda hicho, wameipongeza Serikali kwa uamuzi wake wa kuruhusu
uwekezaji kwenye kiwanda hicho kwani kitanufaisha wakulima wa Chai wa
Halmashauri ya Bumbuli na maeneo yanayozunguka wilaya nzima ya Lushoto na
Korogwe.
“Kwa
niaba ya Wajumbe wa Kamati nichukue fursa hii kuipongeza Serikali kwa kukubali
uwekezaji huu, kwani unakwenda kuleta manufaa makubwa kwa wakulima wa
chai.”Alisema Mhe. Fatma Tawfiq, Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya
Ustawi na Maendeleo ya Jamii.
Mheshimiwa
Tawfiq pia alisema kamati yake itaweka msukumokwa mamlaka husika ili changamoto
zinazokikabili kiwanda ziweze kupatiwa ufumbuzi na hivyo kuwepo na uendelevu wa
utendaji kazi wa kiwanda bila ya vikwazo
Alisema
Kamati imebeba ombi la kiwanda la kurejeshewa umiliki wa shamba la miti la
Sakare ambalo hapo kabla ya kiwanda kusitisha shughuli zake, lilikuwa ndio
tegemeo la uzalishaji wa miti inayotumika kama nishati ya kukaushia chai.
Aidha
Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Riziki Lulida licha ya kupongeza
alishauri uongozi wa kiwanda kutoa ajira kwa makundi mbalimbali wakiwemo wenye
ulemavu.
Akiongea
kwa niaba ya wawekezaji Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi
(WCF), Dkt. John Mduma alisema, kusudio kubwa la kukifufua kiwanda ni
kuwawezesha wananchi wa Lushoto, Bumbuli Korogwe na maeneo jirani kupata kipato
na hivyo kuwainua kiuchumi kwani wengi wanategemea zao hilo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...