Wadau wa Kongamano la Kitaifa la Wanawake Mwaka 2023 lililoandaliwa na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum chini ya Chuo cha Maendeleo ya Jamii Tengeru kwa kushirikiana na LSF na wadau wengine wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya uzinduzi wa kongamano hilo leo Jijini Arusha.

Pichani ni Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mkoani Arusha, Emmanuela Kaganda Mtatifikolo, akimkabidhi Meneja wa Rasilimali na Mawasiliano wa LSF, Jane Matinde, cheti cha shukurani ikiwa ni ishara ya kutambua mchango wa LSF katika kuwezesha Kongamano la Mwaka la Wanawake kwa 2023 lililoandaliwa  Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum chini ya Chuo cha Maendeleo ya Jamii Tengeru kwa kushirikiana na LSF pamoja na wadau wengine.

Mwaka wa pili mfululizo, LSF imeshiriki na kuwezesha Kongamano la Kitaifa la Wanawake lenye lengo la kujadili tafiti mbalimbali zilizofanyika katika masuala ya wanawake ili kubaini hali halisi na kuweka mipango mikakati katika kushughulikia masuala ya wanawake katika nyanja ya kiuchumi, kijamii, na kisiaasa kwa ajili ya kukabiliana na vitendo vya ukatili wa kijinsia.  

"Katika kuendana na ubunifu wa teknolojia ili kuwawezesha wanawake na wasichana kijamii na kiuchumi na kuhakikisha huduma za msaada wa kisheria na upatikanaji wa haki kwa wote, LSF tumezindua Haki Yangu App  inayowezesha kupata elimu ya kisheria, kupata huduma za msaada wa kisheria , kutoa mafunzo maalumu kwa wasaidizi wa kisheria. Kupitia Haki Yangu App, kesi takribani 315 zikiwemo za unyanyasaji wa kijinsia, migogoro ya ardhi, mirathi, migogoro ya ndoa, matunzo kwa watoto zimeripotiwa na kufanyiwa kazi." - Meneja Rasilimali na Mawasiliano LSF, Jane Matinde.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...