Mhandisi Lightness Salema ambaye ni Mkurugenzi wa Kipindi Thamani Madini Limited akimhudumia mteja aliyefika kununua bidhaa  kwenye banda hilo katika maonesho yanayoendelea Mlimani City Dar Es Salaam.
Mkurugenzi wa TWCC Mwanaidi Hamza akizunguma na wajasiriamali hawapo pichani  kwenye Ukumbi wa Mikutano Mlimani City Jijini Dares Es Salaam leo.
Makamu Mwenyekiti  wa TWCC, Victoria Mwanukuzi akikata keki huku shuhudiwa Mlurugenzi wa TWCC Mwajuma Hamza  na wageni wengine meza kuu.Makamu  Mwenyekiti wa TWCC Victoria Mwanukuzi (aliyevaa gauni ya bluu bahari)  na Mkurugenzi wa TWCC Mwajuma Hamza wakiwa kwenye picha ya pamoja na wafanyakazi wa Benki ya wazawa ya Azania ambao wanashiriki kwenye maonesho hayo ya wajasiriamali.


Na Khadija Kalili, Michuzi TV
MAKAMU MWENYEKITI wa  Chama  Cha  Wanawake  Wafanyabiashara  Tanzania (TWCC) Victoria Mwanukuzi  ametoa wito  kwa watanzania wote kuthamini na kununua bidhaa za ndani kwani ndiyo njia kubwa ya kuweza kuzipandisha thamani na kukuza uchumi wa wajasiriamali na wafanyabiashara  kwa ujumla.

Makamu Mwenyekiti Mwanukuzi amesema hayo leo Machi 10,2023 alipokua akizungumza kwenye kongamano la wajasiriamali na wafanyabiashara wanawake katika Ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es  Salaam.

 "Tumekutana leo ikiwa ni katika muendelezo wa kusherehekea siku ya Mwanamke Duniani ambayo huadhimishwa Machi 8 ya kila mwaka....,siku hii sisi tumeiita siku ya wajasiriamali wa Afrika na bado tunaendelea kusherehekea pamoja hivyo nawasisitiza tupende kununua bidhaa za nyumbani kwa sababu zina ubora madhubuti kushinda hata hizo bidhaa na ni za asili" amesema.

"Tuhamasishane kupenda vya nyumbani mimi binafsi nikiingia kufanya manunuzi  kwenye maduka makubwa 'Super Market' huwa nanunua bidhaa zilizoandikwa Made in Tanzania yote hii ni kwa sababu ya kuwa na uzalendo" amesema Mwanukuzi.

Kwa upande wake, Mhandisi Lightness Salema ambaye pia ni miongoni mwa wajasiriamali amesema kuwa wakati umefika wa mjasiriamali ili anyanyuke lazima ajinyanyue mwenyewe ndipo atainuliwa na kusogezwa huku akisisitiza  lazima mwanamke awe mwaminifu kwenye biashara kwa ujumla.

Naye, Mkurugenzi wa TWCC Mwajuma Hamza  amesisitiza kuwa hivi sasa tunaelekea katika soko huru la Afrika  hivyo wajasiriamali ni wajibu wao kujituma na kujikuza ili kuweza kukabiliana na ushindani wa biashara wakati utakapo fika licha ya kuwa wanakabiliana na changamoto mbalimbali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...