Tamasha hilo, litawakutanisha wanamuziki wakongwe wa muziki wa taarab wakiongozwa na Malkia Khadija Kopa, Sabaha Salum Muchacho, Leyla Rashid na Mc Du, Ambao watapanda Jukwaani siku hiyo kukonga nyoyo za wapenzi wa taarab asilia na fedha zitakazopatikana kutokana na viingilio, zitapelekwa kwenye vifaa tiba kwa ajili ya watoto njiti Zanzibar.
Tamasha hilo linakwenda sambamba kabisa na maadhimisho ya Siku ya Mwanamke Dunia ambayo huadhimishwa kila ifikapo Machi 8, ya kila mwaka Duniani kote.
Mgeni rasmi katika tamasha hilo, anatarajiwa kuwa ni Mke wa Rais wa Zanzibar, Mama Mariam Mwinyi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...