Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Daniel Chongolo amesema Tanzania haina mzigo mkubwa wa Madeni kama ilivyo kwa mataifa mengine ya Afrika Mashariki, huku akiwashangaa watu wanaobeza mpango wa Serikali kukopa Fedha Nje ya Nchi.

Chongolo ameyazungumza hayo leo Machi 01, 2023 wakati wa kikao cha shina namba 6 Katika kata ya Ulemo, Wilaya ya Iramba ikiwa ni Siku ya Tatu ya Ziara yake mkoani Singida.

" Hatua ya Serikali kukopa ni kuendelea Kuijenga Tanzania ili iwe imara Kiuchumi kama ilivyo kwa mataifa yaliyopiga hatua Kimaendeleo",alibainisha Chongolo.

Amesema yapo mafanikio mengi ya kiuchumi ikiwemo sekta ya Elimu na Miundombinu ambayo serikali ilikopa zamani na imeshamaliza kulipa, lakini hadi sasa Watanzania wanaendelea kufaidika

Chongolo ametoa rai kwa Jamii kuacha maneno ya watu ambao haiwatakii mema nchi yetu,amesema nchi yetu inakopa na nchi nyigine zote zinazotuzunguka zinakopa, na nchi myingine zote duniani zinakopa zinapokuwa na masuala mahususi ambayo wanadhani kwa kupata fedha na kuyatekeleza yana tija kwa wananchi wake.

Kwa Upande wake Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Sophia Mjema, amewaasa viongozi wa Chama hicho katika ngazi zote, kuendelea kueneza Sera za CCM kwa Vitendo ikiwa ni pamoja na kuweza kuisemea na kuisimamia Miradi inayofanywa na Serikali ya Chama Cha Mapinduzi inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.

Katibu mkuu wa CCM Ndugu Danie Chongolo ameambatana na Katibu wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa itikadi na Uenezi Ndugu Sophia Mjema na Katibu  na Katibu wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa Oganaizesheni
Ndugu Issa Haji Ussi Gavu.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Daniel Chongolo akipata maelezo kutoka kwa Mganga Mfawidhi ya Hospitali ya Kiomboi Daktari Abel Mafuru ya vifaa tiba vya kisasa katika wodi za dharura na la wagonjwa mahtuti Wilayani Iramba mkoa wa Singida.


Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Daniel Chongolo akiteta jambo na Mbunge wa Jimbo la Iramba Ndugu Mwigulu Mchemba (kushoto) wakati wa kikao cha wanachama wa CCM wa shina namba 6, Tawi la Ulemo Kata ya Ulemo wilayani Uramba, katikati ni Mwenyekiti wa shina hilo Ndugu Evangelina Petro Samuel.

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Ndugu Sophia Mjema akihutubia wakazi wa shina namba 6, Ulemo wilayani Iramba mkoa wa Singida
Wanachama wa CCM wa shina namba 6, Tawi la Ulemo Kata ya Ulemo wilayani Uramba wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Daniel Chongolo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...