Na Khadija Kalili
MAHAKAMA ya Wilaya ya Kibaha Mkoani Pwani imemuhukumu Dickson Chilongola (37) kabila Mkaguru ambaye ni fundi wa kuchomelea vyuma ambaye ni mkazi wa Zegereni Mlandizi Wilayani Kibaha Mkoani Pwani hukumu ya kwenda jela maisha , viboko 12 na kulipa fidia ya Mil.2, Hukumu hiyo imetolewa baada ya kupatikana na hatia ya kumbaka mtoto wake wa kufikia mwenye umri wa miaka 10 (jina limehifadhiwa)

Hukumu hiyo ya kesi ya jinai namba 13/2023 imetolewa leo Aprili 28, 2023 na Mheshimkwa Hakimu Judith Lyimo wa Mahakama ya Wilaya ya Kibaha Mkoani Pwani.

Hukumu hiyo imetolewa baada ya kusikiliza ushahidi wa pande zote, Mheshimiwa Hakimu Lyimo amesema kuwa amemtia hatiani mshitakiwa huyo kwa mujibu wa kifungu 130 (1), (2) (e) na kifungu 131 (1) cha kanuni ya adhabu sura ya 16 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2022.

Aidha katika hukumu hiyo imeelezwa kuwa mtuhumiwa ametenda kosa hilo mnamo tarehe 01/02/2023 majira ya usiku mtaa wa Zegereni, Wilaya ya Kipolisi Mlandizi kwa kuingia chumbani kwa mtoto huyo kisha kumfanyia kitendo hicho cha kikatili.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...