Na.Khadija Seif, Michuzi TV
WAZIRI wa Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt.Pindi Chana anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye kilele cha Usiku wa Tuzo za muziki (TMA) Aprili 29,2023 Ukumbi wa Superdome Masaki Jijini Dar es salaam.

Akizungumza na Wanahabari Leo Aprili 27,2023 Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa Taifa (BASATA) Dkt.Kedmon Mapana amesema mchakato wa tuzo ulizunduliwa rasmi mapema mwezi Februari 2023 na ukawataka wasanii kupendekeza kazi zao ziingie kwenye Kinyang'anyiro hicho cha tuzo kwa mwaka 2023.

"Wasanii wengi waliojitokeza kupendekeza kazi zao ambapo kwa mwaka 2023 zaidi ya Kazi 1700 ziliweza kukusanywa ."

Hata hivyo Mapana amesema Usiku huo ni mahususi kwa watu mahiri zaidi pia akaongeza kuwa jumla ya tuzo 52 zitatolewa siku hiyo.

"Tutakuwa na vyeti vya taasisi ambazo zimekuwa zikitoa mchango mkubwa katika muziki pia Usiku huo watatambuliwa pamoja na wasanii ambao wataibuka washindi kwenye vipengele vya tuzo watapatiwa tuzo zao."

Aidha Mapana amewaambia wasanii na wadau wa Sanaa kujitokeza kwa wingi mapema Aprili 28,2023 katika ukumbi wa "Superdome" kwa ajili ya Semina kuelekea Kilele cha Usiku wa tuzo hizo.

Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa Taifa Dkt.Kedmon Mapana akizungumza na Wanahabari leo Aprili 27,2023 kutoa taarifa rasmi ya maandalizi ya Usiku wa Tuzo za muziki nchini (TMA) zinazotarajiwa kufanyika Aprili 29,20223  Ukumbi wa Superdome Masaki Jijini Dar es salaam huku mgeni rasmi akitarajiwa kuwa Waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo  Dkt.Pindi Chana

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...