Na Shamimu Nyaki

Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Hamis Mwinjuma amesema katika Mtaala mpya wa masomo kwa ngazi zote za Elimu nchini, Michezo na Sanaa imekuwa somo la kufundishwa shuleni na lipo pia katika tahasusi za kidato cha tano hadi chuo Kikuu.

Mhe. Mwinjuma amesema hayo Juni 10, 2023 Jijini Dar es Salaam wakati wa mahafali ya kidato cha IV na VI ya Shule ya Academic International Secondary School, ambapo amesema Serikali inaendelea kuweka mazingira bora ya Elimu nchini ikiwa ni pamoja na kuongeza miundombinu na kuboresha iliyopo.

"Elimu ni ufunguo wa maisha, lakini pia Sanaa, Utamaduni na Michezo ni Sekta ambazo katika dunia la leo zina mchango mkubwa katika ajira na kujitegemea, hivyo ni lazima tutoe nafasi kwa watoto wetu kujishughulisha na sekta hizi" amesisitiza Mhe. Mwinjuma.

Aidha, ametoa wito kwa shule binafsi nchini kushiriki katika michezo ya UMITASHUMTA na UMISSSETA kama ambavyo Shule za Serikali zinavyoshiriki.




 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...