Na Mwandishi Wetu,Michuzi TV- Kigoma
KATIBU
 Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM)Daniel Chongolo  amesema Chama hicho 
kinaelekeza Serikali  kuisukuma na kuongeza spidi katika kuhakikisha 
mjadala wa uwekezaji katika Bandari ya Dar es Salaam unafika mwisho ili 
wananchi waanze kuona matokeo yake.
Chongolo ameyasema hayo leo 
Julai 26,2023 wakati akizungumza na wananchi wa Mkoa wa Kigoma kupitia 
mkutano wa hadhara uliofanyika Uwanja wa Mwanga Center ambapo ametumia 
nafasi hiyo kuitaka  Serikali isiingie kwenye maneno ya siasa na badala 
yake wasimame kwenye hoja na hatimaye bandari iongeze ufanisi.
"Tunanachotaka
 ni kuona bandari inaongeza ufanisi,inaletea matokeo na inachangia pato 
kubwa la Taifa na kuongeza tija kwa nchi ya  kuwahudumia Wananchi na sio
 vinginevyo.Mambo yote ya maneno maneno,siasa hizi tusizipe nafasi.
"
 Sisi ndio tumepewa dhamana ya siasa,sisi tunakuja kuzungumza na 
wanasiasa wenzetu na Watanzania waliotupa dhamana,Serikali mambo yao ni 
ya kutenda na kuleta matokeo,na wasifanye mchezo hata kidogo kutosimamia
 maslahi ya nchi kwa kila wanachokifanya’’,amesema Chongolo.
Aidha
 Chongolo alieleza hatua kwa hatua  kuhusu uamuzi wa Serikali kuingia 
makubaliano ya uwekezaji wa kuboresha uendeshaji wa Bandari ya Dar es 
Salaam huku akifafanua lengo kuu ni kuhakikisha bandari hiyo inatoa 
huduma kwa ufanisi mkubwa.


 
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...