Kaimu Mkurugenzi Mkuu CPA Anthony Kasore  akizungumza na waandishi katika moja ya banda katika Maonesho ya 47 ya Biashara Kimataifa Dar es Salaam yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Sabasaba Jijini Dar es Salaam.




Baadhi ya Picha ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa VETA  katika Mabanda ya VETA.

*Serikali imewekeza nfuvu ya kutosha katika kuwafikia watanzania

Na Chalila Kibuda, Michuzi TV
MAMLAKA ya Elimu ya Mafunzo na Ufundi Stadi (VETA) imesema vijana wa kitanzania itumie fursa ya mafunzo ya ufundi stadi kutokana na kuwepo kwa ajira katika mapinduzi ya viwanda nchini.

Hayo ameseyasema Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa VETA CPA Anthony Kasore wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Banda la VETA kwenye maonesho 47 ya Biashara Kimataifa Dar es Salaam (DITF) yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Sabasaba Jijini Dar es Salaam.

Kasore amesema kuwa serikali imewekeza nguvu katika ujenzi wa vyuo mafunzo ya ufundi stadi katika kuhakikisha vijana wanapata ujuzi wa kuweza kuajiriwa na kujiajiri pasipo kuwepo kwa changamoto.

Amesema VETA inatarajia kujenga vyuo 64 ikiwemo kimoja cha Mkoa wa Songwe na vingine vyote vya wilaya.

Aidha amesema Serikali ya awamu ya Sita ya Rais Samia Suluhu Hassan iko bega kwa bega na VETA katika kuwapatia vijana ujuzi waweze kutengeneza ajira na maendeleo kwa ujumla.

Kasore amesema kuwa katika utoaji wa mafunzo kumekuwa na ubunifu ambapo wabunifu walimu na wanafunzi kazi ya VETA ni kuwashika mkono kwa kuwa na miliki ili watu wengine wasije wakazifanyia biashara.

Kasore amesema kuwa wenye viwanda na wawekezaji wasipate changamoto ya nguvu kazi kutokana na nguvu kazi hiyo imeshazalishwa na VETA.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu amesesma VETA inashirikiana na Costech katika kuhakikisha wabunifu wanakuwa wanatambuliwa na kuweza bunifu hizo kwenda mbali zaidi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...