
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda leo Julai 17, 2023 jijini Dar es Salaam amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia Nchini Tanzania Bw. Nathan Belete na ujumbe wake.
Kikao hicho kilikuwa na lengo la kujadili mpango pendekezwa wa utekelezaji wa mageuzi ya Elimu na ushirikiano na Benki ya Dunia katika utekelezaji huo.
Aidha wamekubaliana kuboresha miradi ya BOOST na SEQUIP ili iweze kukidhi kuwezesha mahitaji ya utoaji elimu ujuzi pamoja na kujadili maendeleo ya Miradi mingine katika ngazi ya elimu ya ufundi.





Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...