Mabingwa wa ligi kuu ya Morocco, AS FAR Rabat imemtangaza aliyekuwa kocha wa Yanga SC, Nasreddine Nabi kuwa kocha mkuu wa klabu hiyo kwa mkataba wa miaka miwili wenye kipengele cha kuongeza mmoja zaidi.

Nabi ameondoka Yanga baada ya kufanikiwa kuiwezesha timu hiyo kutinga fainali kwa mara ya kwanza Kombe la Shirikisho barani Afrika ambapo aliondoka kutokana na mkataba wake kufikia tamati.

Kocha huyo ilitegemewa atakuwa kocha wa Kaizer Chief lakini matumaini iligonga mbwa baada ya miamba hiyo ya Madiba kumtangaza kocha mwingine na inasemekana walishindwana na Nabi kwenye upande wa masilahi.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...