NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

JAMII imetakiwa kuachana na imani potofu zinazomkandamiza mwanamke ili chaguzi zijazo, wanawake wengi wajitokeze kwa wingi katika kugombea uongozi kwenye nafasi mbalimbali kwani uwepo wao kwenye uongozi inaleta chachu ya maendeleo kwenye jamii.

Ushauri huo umetolewa leo Agosti 30,2023 katika Semina za Jinsia na Maendeleo (GDSS) ambapo walikuwa wanajadili nafasi ya mwanamke katika ushiriki kwenye uongozi.

Akizungumza wakati akiwasilisha mada, mwezeshaji Bi. Clara Mcharo amesema kuwa jamii imekuwa haina imani na wanawake katika uongozi kutokana na tamaduni zilizopo kwenye jamii ambazo zinaamini kuwa mwanamke hawezi kuwa kiongozi.

Amesema iwapo dini zetu zikiwashirikisha wanawake katika uongozi basi jamii pia itapata uelewa mkubwa katika kuamini wanawake wanaweza hivyo kuwapa nafasi kwenye uongozi ili kuonesha uwezo wao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...