Wizara ya Kilimo na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) wakionesha hati za makubaliano kwa ajili ya Vijana wa Program ya BBT kupata mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa kwa kushudiwa na Rais na Amir Mkuu Dkt.Samia Suluhu Hassan.
Wizara ya Kilimo na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) wakisiani makubaliano kwa ajili ya Vijana wa Program ya BBT kupata mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa

Wizara ya Kilimo na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) wakibadilishana hati za makubaliano kwa ajili ya Vijana wa Program ya BBT kupata mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa kwa kushudiwa na Rais na Amir Mkuu Dkt.Samia Suluhu Hassan.

Na Chalila Kibuda, Michuzi TV
JESHI la Kujenga Taifa (JKT) limeingia makubaliano na Wizara ya Kilimo kutekeleza agizo la Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa Program ya Vijana ya Kujenga Keshi iliyobora (BBT).

Akizungumza mara baada ya kuhitimishwa Maonesho Kitaifa ya Kilimo Nane Nane yalifanyika jijini Mbeya Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Meja Jenerali Rajabu Mabele amesema kuwa makubaliano waliongia na Wizara mbili ni kuwachukua vijana walioko katika mradi wa BBT kupata mafunzo ya kuwajenga katika uzalendo na ukakamavu wakiwa katika mashamba kuwa na uvumilivu.

Amesema kuwa vijana wataopata mafunzo watanufaika katika sekta za kilimo pamoja na mifugo kuwa mfano wa kuigwa na vijana wengine kuingia katika sekta hizo.

Meja Jenarali Mabele amesema wametiliana saini mkataba wa mashirikiano katika kutekeleza mradi wa mashamba makubwa kuwezesha vijana kulima, kibiashara kwenye mradi huo Building a Better Tommoow (BBT)

Amesema makubaliano hayo mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Naye Mkuu wa Huduma za Sheria wa Jeshi Kujenga Taifa (JKT) Kanali Projestine Rutaiwa amesema mafunzo ya vijana wa BBT yataratibiwa kwa ushirikiano wa wizara hizo.

Amesema kuwa makabaliano hayo kwa mafunzo watayoyapata yataleta matokeo chanya katika vijana hao kwenda kutekeleza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...