Tanzania na Malawi zimeweka nia ya kushirikiana katika Usafiri kwa Njia ya Barabara, huduma za Bandari katika ziwa Nyasa na Hudumiaji wa mizigo ya Malawi katika Bandari ya Dar es Salaam.
Hayo yamelezwa na Katibu Mkuu anayesimamia Sekta ya Uchukuzi Gabriel Migire kwenya Mkutano uliowakutanisha Makatibu wakuu wa sekta ya Uchukuzi toka Tanzania na Malawi lengo la Mkutano huu ni uboresha usafirishaji kwa njia ya Barabara,
“huduma za Bandari kwa ziwa Nyasa kwakua ziwa hili lipo katika pande Mbili yaani Tanzania na Malawi pia kuendelea kuwashawishi kutumia Bandari ya Dar es Salaam”Alisema Migire.
Kwa Upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Usafirishaji wa Umma kutoka Malawi Hastings Chiudzu amesema kuwa ni muhimu kwa wizara hizi kushirikiana na kuondoa changamoto mbalimbali za usafirishaji
Pia katibu Mkuu huyo amesema ataendelea kuwashawishi wafanyabishara wa Malawi kuendelea kutumia Bandari ya Dar es Salaam kwani Bandari hii ianautaratibu mzuri wa kushusha na kupakia Mizigo.
Wataalam hao kutoka Malawi walitembelea Ujenzi wa SGR na Bandari ya Dar Es Salaam na kuipongeza serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutekeleza Mradi huo Mkubwa wa Ujenzi wa SGR pamoja na upanuzi wa Bandari.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...