
Madaktari wazawa Hospitali ya Taifa Muhimbili wanaendelea kufanya upasuaji wa kupandikiza figo ambapo wagonjwa 12 kuanzia leo watapata huduma hiyo sita kati yao watafanyiwa Upanga kwa njia ya kawaida na sita watafanyiwa wiki ijayo huko Mloganzila kupitia mfumo wa matundu madogo.
Akizungumza na Waandishi wa Habari Jijini Dar Es Salaam, Mkurugenzi wa Huduma za Tiba wa Hospitali hiyo Dkt. John Rwegasha amesema huu ni mwendelezo wa utoaji huduma za kibingwa nchini unaofanywa na madaktari wazawa ambao sasa wana ujuzi wa kutoa huduma hizo.

Tangu kuanzishwa huduma hii Hospitali ya Taifa Muhimbili imepandikiza wagonjwa 75 mwaka 2017.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...