Njombe

Watu watatu wanaodaiwa kuwa ni Majambazi,wamevamia kituo cha mafuta cha Orexy mkoani Njombe usiku wa kuamkia  Septemba 3,2023 na kujaribu kuiba, zoezi ambalo halikufanikiwa baada ya polisi kuwasili kwa wakati eneo la tukio na kufanikiwa kuwadhibiti wahalifu hao.

Kamanda wa polisi Mkoa wa Njombe Kamishna msaidizi wa Polisi John Makuri Imori amesema watu hao watatu waliokamatwa baada ya kujeruhiwa na polisi katika majibizano ya risasi,wanahusika na tukio lililotokea siku chache zilizopita la kuvamia nyumbani kwa wakala wa fedha Golden Luoga na kuua watu wawili akiwemo mfanyabiashara huyo pamoja na kaka yake Faraja Luoga.

"Askari waliposhtuka kwamba hawa wanakimbia wakapiga risasi juu ili wasimame na wao wakajibu na walipokuwa wakijibu bahati mbaya na askari wa kwetu nao wakawajeruhi hawa watatu na katika eneo la tukio tumeweza kukamata silaha mbili za moto"amesema Kamanda Makuri

Kamanda Makauri ameongeza kuwa baada ya tukio la mauaji ya wafanyibiashara mkoani humo polisi walijiimarisha kwa kuongeza nguvu kazi kwenye doria za usiku na hatimae siku ya tarehe moja mwezi Septemba walifanikiwa kumnasa mtu moja aliefahamika kwa majina ya Said Mohammed Bakari (52) mkazi wa chamazi Dar es salaam,ambae alikutwa na vitu mbalimbali ambavyo ni mali ya mfanyi biashara alieuliwa katika tukio la uvamizi lililopita.

Aidha kamanda ameeleza kuwa baada ya mahojiano ya kina na mtuhumiwa huyo, alifanikiwa kuwataja wenzie na kisha akaeleeza mipango waliyo nayo ikiwemo kuvamia kituo cha mafuta,mipango iliyowafanya polisi kuweka mtego na kufanikiwa kuwatia mbaroni huku pia wakibaini vitu mbalimbali vilivyokuwa na watuhumiwa hao kuwa ni vya marehemu aliyeuwa kwa risasi hivi karibuni.
"Tumekuta Pos mashine mbili moja ya NMB na beji moja jeusi mali ya Golden Luoga ambaye ni marehemu kwa sasa"alisema Kamanda Makuri



 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...