Na Mwamvua Mwinyi,Pwani

MKE wa mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini,Mama Selina Koka amekubali kuwa mlezi wa Chama Cha Waandishi Wa Habari Wanawake mkoani Pwani, ambapo ameahidi kuwabeba ili kutimiza malengo yao.

Akizungumza na wanachama wa Chama hicho ,ambao alikutana nao kwa mara ya kwanza baada ya kukubali ombi hilo, alieleza waandishi ni kama makundi mengine katika jamii ambayo yanahitaji kujiinua kupitia miradi mbalimbali, biashara na kupitia shughuli zao .

Selina alisema anawaunga mkono waandishi wa habari,na atahakikisha wanajiinua katika Chama chao kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.

"Nimekubali Kuwa mlezi wenu nachosisitiza ni Umoja, Mshikamano ,msiniangushe, naamini tutafanya mengi ,"Simamieni katiba yenu,shirikianeni katika mambo ya Chama na ya kijamii ,saidianeni na mjiepushe na kukwazana ,kila mmoja aondoe tofauti zake kwa mwenzake na mtafika"alishauri Selina.

Vilevile Selina anawaomba kujiwekea malengo kwa juhudi na mikakati madhubuti, na kwa dhana hiyo ameambatana na Ujumbe kutoka Taasisi ya kifedha ya Azania , ili kuwaunganisha kuweka akiba kwa manufaa Yao.

Nae Neema Masanja na Nuru Athuman maofisa kutoka Taasisi ya kifedha ya Azania Tawi la Tegeta walieleza,ni bank ambayo haina makato ya kumuumiza mtanzania wala mwanamke.

Nuru alifafanua, ni wakati wa akinamama kunufaika na ujio wa akaunti na mkopo mahsusi kwa wanawake ya MWANAMKE HODARI ambapo,riba yake ni nafuu asilimia moja kwa mwezi na haina makato na unafungua akaunti bure.

Awali Mwenyekiti wa Chama Cha Waandishi Wa Habari Wanawake mkoani Pwani, Mwamvua Mwinyi, alimshukuru Mama Koka kwa kukubali ombi hilo la Ulezi.

Alieleza kwamba, Chama hicho ,kimeanza rasmi Michakato ya kuwa chama kamili 2013, kina viongozi wanne,wanachama 15 ,kwa miaka mitano kilisimama kwa muda kujiweka sawa na sasa kimekuja kivingine.

"Ongezeko la vitendo vya ukatili kwa watoto ikiwemo kubakwa ,kulawitiwa, mimba za utotoni pamoja na baadhi yao kunyimwa haki ya Elimu ,linaonekana kuwa kubwa, tumekuwa tukishuhudia baadhi ya watoto wakinyimwa haki zao za msingi na wengine kulawitiwa ama kubakwa huku mijibaba iliyohusika kutuhumiwa kutenda vitendo hivyo ikiona ni jambo la kawaida suala ambalo linatakiwa kulipiga vita kwa nguvu zote,pasipo kulifumbia macho hata kidogo "

Mwamvua anaeleza,masuala hayo ndio yaliyowagusa na kuwashawishi kuanzisha chama ili kuweza kushirikiana na jamii,dawati la jinsia,ustawi wa jamii kwa lengo la kutimiza adhma ya kutokomeza vitendo hivyo.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...