TAASISI  ya Elimu Tanzania (TET) kwa kushirikiana na Kituo cha Urithi wa  Ukombozi Bara la Afrika wanashiriki Tamasha la 42 la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni linalofanyika katika Taasisi ya Sanaa na Utamaduni (TaSuBa)  mjini Bagamoyo lililoanza kuanzia Oktoba 26 mwaka 2023 .

Katika tamasha hilo wadau mbalimbali wameombwa kutembelea katika banda la TET kwa lengo la kuangalia machapisho mbalimbali yanayotolewa na taasisi hiyo.

Akizungumza katika maonesho hayo,Ofisa Uhusiano  wa TET  Angella Msangi ameleeza  katika tamasha hilo , wadau watapata kuona vitabu vya historia vilivyoandaliwa  na TET vilivyoshirikisha wataalamu  bobezi katika kufundisha somo  la historia kutoka Taasisi mbalimbali.

“Mje mjione mauudhui yaliyomo kwenye vitabu hivyo ambayo yamelenga kumwezesha mwanafunzi kupata umahiri wa kuijua historia ya nchi yake na ya mahusiano ya Tanzania na nchi nyingine”. Amesema  Anngella.

Pia, mwanafunzi atapata nafasi ya kujua  historia iliyo nje ya Tanzania na hasa bara la Afrika na  kufahamu masuala mbalimbali.

Pamoja na hayo, katika tamasha hilo wananchi wataweza kuona machapisho mbalimbali yanayotolewa  na kufahamu kazi zinzofanywa na TET kwa ujumla.

Tamasha hilo linatarajia kumalizika Oktoba 28, 2023 ambapo washiriki mbalimbali kutoka katika taasisi za binafsi za Serikali na nje ya nchi  zinaashiriki.








Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...