Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bi Mary Maganga akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari juu ya Kikao cha Maandalizi wa Mkutano wa (COP28) utakaofanyika Dubai,Umoja wa  Falme za Kiarabu Novemba 30 hadi Decemba 12,2023 
Mshauri wa  Rais katika masuala ya Mazingira na Mabadiliko ya Tabianchi Dkt. Richard Muyungi akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari juu ya Mkutano wa (COP28) utakaofanyika Dubai,Umoja wa Falme za Kiarabu 
Baadhi ya washiriki wa kikao hicho cha maandalizi ya Mkutano wa (COP28)utakaofanyika  Novemba 30 hadi 12Decemba 2023 Dubai,Umoja wa Falme za Kiarabu 


Vero Ignatus,Arusha.
 
Kikao cha  Kitaifa cha Wadau wa maandalizi ya mkutano wa nchi wananchama wa  Wanachama wa Kimataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi (COP28) utakaofanyika Dubai,Umoja wa  Falme za Kiarabu umefunguliwa leo 26 Oktoba2023 Jijini Arusha ukiwa na lengo la kupata msimamo mmoja wa nchi juu ya Mabadiliko ya tabianchi. 

Akifungua kikao hicho Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bi Mary Maganga  amesema kuwa  Serikali  imejipanga vizuri  katika Sera za utunzaji wa Mazingira kulingana  na mabadiliko ya tabianchi katika maeneo ya Kilimo na Uchumi wa Buluu, 

Bi. Maganga amesema kuwa kwa masuala ya Kisera tayari Serikali  imeshaandaa miongozo, kanuni na sera ambazo zitasidia nchi kukabiliana na mabadiliko hayo  ambapo ililizinduliwa 2021,pamoja na sera ambayo itakayosaidia nchi kupunguza uzalishaji wa gesi joto kwani itakuwa ni fursa kwa nchi kuelezea mchango huo
 
Kwa upande wake Mshauri wa  Rais katika masuala ya Mazingira na Mabadiliko ya Tabianchi Dkt. Richard Muyungi  amesema Tanzania ni  nchi mojawapo katika Bara la Afrika inayokabiliwa na athari za mabadiliko ya tabianchi yakiwemo mafuriko,hivyo

Amesema  kuwa 23-25 walikutana wataalam kujadi masuala Mbalimbali ikiwemo matokeo ya mkutano 27 uliofanyika nchini Misri pamoja na kupitia maandiko mbalimbali yahusuyo mabadiliko ya tabianchi 

"Tunapokwenda kwenye mkutano hii mikubwa ya Kimataifa kama nchi tunatakiwa tujiandae kwa maandiko mbalimbali kutoka katika Sekta za Serikali, binafsi na CSO kwani tutakuwa na shughuli mbalimbali za kuelezea juu ya mabadiliko ya tabianchi. 

kuwa upo umuhimu mkubwa wa kuchukua hatua ili kukabikiana na mabadiliko ya Tabianchi kwani nchi ina sera ambazo wanasimami ikiwemo mokakati mingine ya kisekta inatekelezwa ili kupunguza uchahafuzi wa mazingira sambamba na mabadiliko ya tabianchi. 

Kwa upande wake Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Dkt. Omar Dadi Shajak amesema madhumuni ya kikao hicho ni kujiandaa kwa ajili ya Mkutano wa COP28 huku masuala ya Uchumi wa Buluu yatakuwa ni ajenda muhimu.

Nae, Kaimu Mkurugenzi wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Paul Deogratius ametaja lengo kuu la wajumbe hao kukutana jijini Arusha ni kujadili kwa pamoja yaliyojiri kwenye COP27 iliyofanyika nchini Misri mwaka 2022 mafanikio, changamoto na mwelekeo kuelekea COP28.

Aidha Mkutano huo wa ( COP28) utakaofanyika Dubai,Umoja wa Falme za Kiarabu kuanzia Novemba 30 hadi Decemba 12,2023 Ambapo msimamo wa nchi ni kuwa na lugha moja katika  suala hilo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...