Na; Mwandishi Wetu – Dar es Salaam

Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Patrobas Katambi amesema Serikali itaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa Watu wenye Ulemavu ili kukuza ustawi wa kundi hilo katika kuchochea shughuli za maendeleo.

Ameeleza hayo katika tamasha la kimataifa la familia yenye furaha la Watu wenye Uziwi na usikivu hafifu, lililofanyika jijini Dar es Salaam ambapo tamasha hilo lilihusisha pia mshindano la kumsaka mrembo, mtanashati pamoja na mwanamitindo bora duniani mwenye Uziwi.

Aidha, Mhe. Katambi amesema kuwa Mhe. Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan anawapenda na kuwajali Watu wenye Ulemavu na ndio maana serika anayoiongoza imeunda wizara mahususi ili kusimamia watu wenye ulemavu.

Amebainisha kuwa Serikali inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan imefufua vyuo vya Watu wenye Ulemavu kwa kutumia Tsh. Bilioni 3.4 kukarabati miundmbinu ambayo imechakaa katika vyuo 6.

Pia ameeleza kwa mwaka huu wa fedha 2023-2024 serikali imetenga Bil. 3 kwa ajili ya ujenzi wa vyuo vipya vitatu vya ufundi stadi ili kuongeza udahili wa vijana wenye Ulemavu kupata ujuzi utakaowawezesha kujiajiri au kuajiriwa.

Vile vile, katika kuimarisha utambuzi wa mapema wa watoto wenye Ulemavu, serikali imeandaa mwongozo wa utambuzi wa mapema na afua staki kwa watoto wenye Ulemavu.

Sambamba na hayo, amesema kuwa Serikali imeendelea kuwawezesha Watu wenye Ulemavu kiuchumi kama ilivyoainishwa katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020 kwa lengo la kuwawezesha kujikwamua kiuchumi.

Tamasha hilo limehusisha washiri zaidi ya 200 kutoka mataifa ya Afrika Kusini, Australia, Belarus, Brazil, Ethiopia, Falme za Kiarabu, Guyana, Haiti, Hispania, India, Iran, Italia, Kenya, Kongo DRC, Malasia, Macedonia, Marekani, Mexico, Misri, Morocco, Msumbiji, Nigeria, Pakistan, Poland, Romania, Rwanda, Senegal, Siera Leone, Sudan Kusini, Thailand, Tunisia, Jamhuri ya Czechoslovakia, Ufaransa, Uganda, Ujerumani, Ukraine, Urusi, Zambia, Zimbabwe na wenyeji Tanzania.








 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...