Na; Mwandishi
Wetu – Dar es Salaam
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe.
Patrobas Katambi amesema Serikali itaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa Watu
wenye Ulemavu ili kukuza ustawi wa kundi hilo katika kuchochea shughuli za
maendeleo.
Ameeleza hayo katika tamasha la kimataifa la familia yenye furaha la
Watu
wenye Uziwi na usikivu hafifu, lililofanyika jijini Dar es Salaam ambapo
tamasha hilo lilihusisha pia mshindano la kumsaka mrembo, mtanashati
pamoja na mwanamitindo bora duniani mwenye Uziwi.
Aidha, Mhe. Katambi amesema kuwa Mhe. Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan anawapenda
na kuwajali Watu wenye Ulemavu na ndio maana serika anayoiongoza imeunda wizara
mahususi ili kusimamia watu wenye ulemavu.
Amebainisha kuwa Serikali inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan imefufua
vyuo vya Watu wenye Ulemavu kwa kutumia Tsh. Bilioni 3.4 kukarabati miundmbinu
ambayo imechakaa katika vyuo 6.
Pia ameeleza kwa mwaka huu wa fedha 2023-2024 serikali imetenga Bil. 3 kwa
ajili ya ujenzi wa vyuo vipya vitatu vya ufundi stadi ili kuongeza udahili wa
vijana wenye Ulemavu kupata ujuzi utakaowawezesha kujiajiri au kuajiriwa.
Vile vile, katika kuimarisha utambuzi wa mapema wa watoto wenye Ulemavu,
serikali imeandaa mwongozo wa utambuzi wa mapema na afua staki kwa watoto wenye
Ulemavu.
Sambamba na hayo, amesema kuwa Serikali imeendelea kuwawezesha Watu wenye
Ulemavu kiuchumi kama ilivyoainishwa katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya
mwaka 2020 kwa lengo la kuwawezesha kujikwamua kiuchumi.
Tamasha hilo limehusisha washiri zaidi ya 200 kutoka mataifa ya Afrika Kusini,
Australia, Belarus, Brazil, Ethiopia, Falme za Kiarabu, Guyana, Haiti, Hispania,
India, Iran, Italia, Kenya, Kongo DRC, Malasia, Macedonia, Marekani, Mexico,
Misri, Morocco, Msumbiji, Nigeria, Pakistan, Poland, Romania, Rwanda, Senegal,
Siera Leone, Sudan Kusini, Thailand, Tunisia, Jamhuri ya Czechoslovakia,
Ufaransa, Uganda, Ujerumani, Ukraine, Urusi, Zambia, Zimbabwe na wenyeji
Tanzania.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...