SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limefanikiwa kupata kombe la mshindi wa pili kwa mchezo wa kuvuta kamba katika mashindano ya SHIMMUTA ambayo yamefanyika Jijini Dodoma.

Akizungumza na Waandishi wa habari Nov 25,2023, Mwenyekiti wa michezo wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) Bw. Lucas Gwila amesema kuwa moja ya sababu ya mafanikio yao kufika hatua ya fainali katika mashindano hayo ni suala la nidhamu kwa timu nzima pamoja na ushirikiano.

"Siri ya mafanikio yetu ni suala la nidhamu, ushirikiano na ushiriki wa mara kwa mara kwenye mabonanza yanayofanyika kwenye taasisi, kufanya mazoezi na kuchagua wachezaji wazuri". Amesema

Aidha Bw. Gwila amesema kuwa moja ya sababu iliyotia chachu mafanikio yao ni pamoja na kuwa na mbinu za ushindani, na kushindwa kwao kutwaa ubingwa kumesababishwa na kuzidiwa mbinu, ameahidi kwa mashindano yajayo watajitahidi kuchukua ubingwa kutokana na uzoefu walioupata.

"Mwakani timu yetu ya mashindano ya kamba ya TBS, naahidi tunaenda kuchukua ubingwa,nadhani wametuzidi kwenye mbinu ndogo ndogo". Ameeleza Bw. Gwila.

Amesema mashindano ya SHIMMUTA yanazidi kuwa bora zaidi kila mwaka ambapo kwa mwaka 2023 imekadiriwa zaidi ya watu 4000 wamejitokeza kuhudhuria na kushiriki katika mashindano hayo.

SHIMMUTA ni miongoni mwa Mashirikisho manne ya michezo yaliyoanzishwa na Serikali ya Awamu ya Kwanza iliyoongozwa na Hayati Baba wa Taifa, Mwl. Julius Kambarage Nyerere mnamo mwaka 1967 ambapo yanahusisha Mashirika ya Umma, Taasisi na makampuni binafsi Tanzania katika michezo kwa kusudi la kujenga mahusiano mema kitaasisi.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...