Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amemteua Bw. Mohamed Malick Salum kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC). Kabla ya uteuzi huu Bw. Salum alikuwa Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria, Wizara ya Uchukuzi.

Bw. Salum anachukua nafasi ya Bw. Kaimu Abdi Mkeyenge aliyeteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima la Taifa (NIC).

Uteuzi huu unaanza tarehe 14 Novemba, 2023.

Zuhura Yunus
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...